KM apendekeza muda wa ulinzi amani Ethiopia na Eritrea uongezwe
Ripoti ya KM juu ya hali mipakani kati ya Ethiopia na Eritrea imependekeza Baraza la Usalama liongeze kwa miezi sita ziada operesheni za ulinzi wa amani za UM katika eneo hilo.
Ripoti ya KM juu ya hali mipakani kati ya Ethiopia na Eritrea imependekeza Baraza la Usalama liongeze kwa miezi sita ziada operesheni za ulinzi wa amani za UM katika eneo hilo.
Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limepokea kutoka idara inayohusika na misaada ya kiutu ya Umoja wa Ulaya (EU) msaada wa dola milioni 1.3 ulikusudiwa kuhudumia wahamiaji wa Sahara ya Magharibi waliopo Algeria.
Didier Drogba, mchezaji mashuhuri wa mpira kutoka Cote d’Ivoire anayechezea timu ya Chelsea ya Uingereza, na kuongoza kwa kufunga magoli mengi zaidi kushinda wachezaji wengine Ulaya hivi sasa, ameteuliwa na Shirika la UM juu ya Miradi ya Maendeleo (UNDP) kuwa Balozi Mfadhili, atakayesaidia kwenye zile juhudi za kuhamasisha umma wa kimataifa kujumuisha mchango wao maridhawa, ili kukamilisha, kwa wakati, yale Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs).
Hivi majuzi, Afrika Mashariki ilikabiliwa na tatizo la mafuriko ya kihistoria yaliotukia baada ya mvua kali kunyesha mwisho wa mwaka 2006. Maafa haya yalisababisha uharibifu mkubwa wa hali na mali, hususan, miongoni mwa wale wahamiaji waliopo mipakani kati ya Kenya na Usomali.
Sehemu ya pili ya makala hii inaendelea na mahojiano aliyokuwa nayo KM mstaafu Kofi Annan na wanahabari wa kimataifa kwenye kikao cha mwisho kabla ya kukhitimisha kazi na Umoja wa Mataifa (UM).
KM mstaafu Kofi Annan, siku chache kabla ya kumaliza uongozi wake wa miaka 10 katika Umoja wa Mataifa, aliitisha kikao cha mwisho cha mahojiano na waandishi habari wa kimataifa waliopo Makao Makuu mjini New York. Alizungumzia masuala mbalimbali na kuchambua taratibu zinazohitajika kutekelezwa ili kuboresha uhusiano wa kimataifa miongoni mwa Mataifa Wanachama.
Ijumanne KM Ban Ki-Moon alizuru Ikulu ya Marekani mjini Washington DC na kufanya mkutano rasmi, wa awali, na Raisi wa Marekani George Bush. Ziara hiyo ilihusika na hishima za kidiplomasia kwa Serekali Mwenyeji wa UM, yaani Serekali ya Marekani, ziara ambayo KM mpya anawajibika kuikamilisha.~
Mapema wiki hii UM ulipeleka tume maalumu ya ukaguzi, kwenye mji wa Mogadishu, Usomali kwa mara ya kwanza tangu Serekali ya Mpito kuchukua madaraka. Dhamira ya ujumbe huo ni kutathminia mahitaji ya misaada ya kiutu kwa raia wa Usomali.
Raisi wa Baraza la Usalama kwa mwezi Januari, Balozi Vitaly Churkin wa Shirikisho la Urusi aliwaambia waandishi habari waliopo Makao Makuu ya UM kwamba wajumbe wa mataifa 15 katika Baraza hilo walikubaliana kupendekeza kwa KM Ban Ki-moon atayarishe haraka tume ya utangulizi itakayozuru Chad na pia Jamhuri ya Afrika ya Kati kwa mashauriano na serekali za mataifa haya mawili. Baadaye KM alitakiwa atayarishe ripoti ya mapema itakaousaidia UM kuandaa operesheni za ulinzi wa amani katika eneo lao.
Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limeanzisha operesheni za kuwahudumia chakula watu 500,000 muhitaji wa eneo la Karamoja, katika Uganda ya kaskazini-mashariki.