Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

KM kuanzisha rasmi mfuko wa ujenzi wa amani

Ijumatano KM Kofi Annan alishiriki kwenye kikao maalumu cha kuanzisha Mfuko wa Ujenzi wa Amani wa UM utakaotumiwa kuyasaidia yale mataifa yanayoibuka kutoka hali ya uhasama kurudisha amani kwenye maeneo yao na kujiepusha na hatari ya kuteleza tena kwenye mapigano, vurugu na machafuko.

Hali ya usalama katika Darfur yazidi kuharibika

Shirika la UM juu ya Huduma za Amani katika Sudan (UNMIS) limeripoti kuwa hali ya usalama katika Darfur ya kusini, inaendelea kuharibika, hususan katika mji wa Gereida, kutokana na mvutano uliojiri na uhasama kati ya makabila yanoishi kwenye eneo hilo. Wakati huo huo kwenye mji wa Um al-Kher, Darfur ya Magharibi imeripotiwa kutukia vifo vya watu walioambukizwa na maradhi ya kipindupindu. Ripoti ya karibuni ya KM imeonya ya kuwayale mashirika yanayohudumia misaada ya kiutu huenda yakafunga operesheni zake pindi hali ya usalama haijadhibitiwa katika eneo kama ipasavyo. ~~

Vikosi vya MONUC kushiriki kwenye doria ya kuulinda mji mkuu wa Congo-DRC

Wanajeshi wa Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, yaani Shirka la MONUC wameanzisha, wiki hii, doria yenye mada isemayo “Kinshasa, mji usio silaha”, kwa makusudio ya kuzuia vikundi vyenye kuchukua silaha kutoaranda randa ovyo na kuzusha fujo na vurugu, hususan katika kipindi ambacho taifa linajiandaa kufanya duru ya pili ya uchaguzi wa raisi mwisho wa Oktoba. Vikosi vya MONUC vinashirikiana kwenye doria hii maalumu na majeshi ya taifa ya Congo-DRC pamoja na vikosi vya polisi vya kutoka Umoja wa Ulaya.

Uchaguzi wa KM mpya wa Umoja wa Mataifa unanyemelea

Ijumatatu tarehe 09 Oktoba (2006) Baraza la Usalama linatazamiwa kupiga kura ya kumteua rasmi KM mpya atakayechukua nafasi ya KM Kofi Annana mnamo mwanzo wa 2007. Baada ya hapo Baraza la Usalama litatuma jina la KM mpya mbele ya Baraza Kuu kuidhinishwa na wawakilishi wa kimataifa.