Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 22 septemba 2019 hadi 30 Septemba 2019. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Mkutano wa vijana wa vijana na mabadiliko ya tabianchi, fursa ya afya kwa wote, mkutano kuhusu fursa ya afya kwa wote, tathimini ya hatua za utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, ufadhili kwa ajili ya maendeleo na tathimini ya mwelekeo wa mkakati wa SAMOA.
MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Kwaheri UNGA74 karibu UNGA75
Hatimaye mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umefunga rasmi pazia lake hii leo na kuashiria kuanza kwa mkutano wa 75 wa Baraza hilo, ambalo ni moja vyombo vikuu vya Umoja wa Mataifa wenye wanachama 193.
Ushirikiano wa kimataifa unasalia kuwa nguzo ya suluhu ya kimataifa-Muhammad
Akitoa taarifa ya kufunga mjadala Mkuu wa wazi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York hii leo Rais wa Baraza Kuu Tijjani Muhammad-Bande amesema ushirikiano wa kimataifa unasalia kuwa nguzo muhimu inayokubalika na kutegemewa katika kutatua changamoto za kimataifa miongoni mwa nchi wanachama.
Asilani hatutotiwa woga na vitisho:China
Katika hotuba yake kwenye mjadala Mkuu wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa siku ya Ijumaa Diwani wa jimbo na waziri wa mambo ya nje wa Uchina ametangaza kwamba nchi yake asilani haitotiwa woga na vitisho au kukubali shinikizo wakati inapokabiliwa na changamoto za ulinzi.
Burundi sasa ni shwari tuungeni mkono katika uchaguzi:Nibigira
Waziri wa mambo ya nje wa Burundi Ezechiel Nibigira ameiambia Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kuwa anakusudia baadaye hii leo kuuleza mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74 pamoja na mambo mengine, kuhusu hatua za maendeleo ambazo Burundi imepiga na pia kuiomba jumuiya ya kimataifa kuiunga mkono nchi yake.
Burundi yataka iondolewe kwenye ajenda ya Baraza la Usalama
Mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74 ukitamatishwa hii leo jiijni New York, Marekani, Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa Burundi Ezechiel Nibigira amehutubia jukwaa hilo akitaka ajenda ya Burundi kwenye Baraza la Usalama iondolewe kwa kuwa hali ya usalama nchini humo ni tulivu.
Vijana mitandao ya kijamii iwe na faida na sio hasara kweny:Ogola
Mitandao ya kijamii ina hatari na athri kubwa zaidi kwa vijana inapotumiwa vibaya amesema balozi mwema wa wakfu wa Umoja wa Mataifa au UN Foundation Philip Ogola.
Tuwajibike wote kudhibiti kuenea kwa nyuklia- Urusi
Urusi imezungumzia mtazamo wake kuhusu hali inayoendelea nchini Iran, mzozo nchini Syria, vibali vya kuingia Marekani kwa maafisa wake wa kibalozi na masuala mengine nyeti kwenye ajenda ya kimataifa.
Nchi 38 zinazoendelea za visiwa vidogo, ni kati ya nchi zilizo hatarini zaidi
Nchi 38 zilizotambuliwa na Umoja wa Mataifa kama nchi zinazoendelea za visiwa vidogo, au SIDS, ni kati ya nchi zilizo hatarini zaidi ulimwenguni. Nchi hizi ambazo ziko kwenye eneo la Karibea, bahari ya Pasifiki, ya Atlantiki, ya Hindi na Bahari ya Uchina ya Kusini zinaathirika na hali inayozidi ya mabadiliko ya tabianchi ulimwenguni ambayo haitabiriki. Pamoja na changamoto za mazingira, SIDS inakabiliwa na seti ya kipekee ya masuala yanayohusiana na udogo na umbali.
Uganda inaendelea kuunga mkono ushirikiano wa kimataifa-Dkt Rugunda
Waziri Mkuu wa Uganda Dkt Ruhakana Rugunda akihutubia mjadala mkuu wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa mkutano wa 74, UNGA74, miongoni mwa mengi, amesema Uganda inaendelea kuunga mkono ushirikiano wa kimataifa kwani ndiyo njia ya kufikia malengo dunia iliyojiwekea.
Tanzania tumedhamiria kubadili maisha ya watu wetu:Kabudi
Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania Profesa Palamagamba John Kabudi amesema Tanzania imedhamiria kubadili maisha ya wananchi wake ikijitahidi kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu SDGs.