Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA

MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
MJADALA MKUU WA UNGA74

Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 22 septemba 2019 hadi 30 Septemba 2019. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu  Mkutano wa vijana wa vijana na mabadiliko ya tabianchi, fursa ya afya kwa wote, mkutano kuhusu fursa ya afya kwa wote, tathimini ya hatua za utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, ufadhili kwa ajili ya maendeleo na tathimini ya mwelekeo wa mkakati wa SAMOA.

Volkan Bozkri, Rais wa mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la UN, UNGA75 akinyanyua rungu kuashirikia kuchukua urais wa kiti hicho, huku Katibu Mkuu Antonio Guterres na Rais aliyemazali muda wake Tijjani Muhammad-Bande wakitazama.
UN WebTV

Kwaheri UNGA74 karibu UNGA75

Hatimaye mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umefunga rasmi pazia lake hii leo na kuashiria kuanza kwa mkutano wa 75 wa Baraza hilo, ambalo ni moja vyombo vikuu vya Umoja wa Mataifa wenye wanachama 193.
 

Wang Yi, waziri wa mambo ya nje wa Jamhuri ya watu wa China akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kikao cha 74
UN Photo/Loey Felipe

Asilani hatutotiwa woga na vitisho:China

Katika hotuba yake kwenye mjadala Mkuu wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa siku ya Ijumaa Diwani wa jimbo na waziri wa mambo ya nje wa Uchina ametangaza kwamba nchi yake asilani haitotiwa woga na vitisho au kukubali shinikizo wakati inapokabiliwa na changamoto za ulinzi.

OCHA/Christian Cricboom

Burundi sasa ni shwari tuungeni mkono katika uchaguzi:Nibigira

Waziri wa mambo ya nje wa Burundi Ezechiel Nibigira ameiambia Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kuwa anakusudia baadaye hii leo kuuleza mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74 pamoja na mambo mengine, kuhusu hatua za maendeleo ambazo Burundi imepiga na pia kuiomba jumuiya ya kimataifa kuiunga mkono nchi yake.

Sauti
2'12"
Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa Burundi Ezechiel Nibigira akihutubia mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74.
UN Photo/Cia Pak

Burundi yataka iondolewe kwenye ajenda ya Baraza la Usalama

Mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74 ukitamatishwa hii leo  jiijni New York, Marekani, Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa Burundi Ezechiel Nibigira amehutubia jukwaa hilo akitaka ajenda ya Burundi kwenye Baraza la Usalama iondolewe kwa kuwa hali ya usalama nchini humo ni tulivu.

Visiwa vya Tuvalu viko katika hatari ya kuongezeka kwa kina cha maji ya bahari kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.
UNDP Tuvalu/Aurélia Rusek

Nchi 38 zinazoendelea za visiwa vidogo, ni kati ya nchi zilizo hatarini zaidi

Nchi 38 zilizotambuliwa na Umoja wa Mataifa kama nchi zinazoendelea za visiwa vidogo, au SIDS, ni kati ya nchi zilizo hatarini zaidi ulimwenguni. Nchi hizi ambazo ziko kwenye eneo la Karibea, bahari ya Pasifiki, ya Atlantiki, ya Hindi na Bahari ya Uchina ya Kusini zinaathirika na hali inayozidi ya mabadiliko ya tabianchi ulimwenguni ambayo haitabiriki. Pamoja na changamoto za mazingira, SIDS inakabiliwa na seti ya kipekee ya masuala yanayohusiana na udogo na umbali.