Mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 25 septemba 2018 hadi Oktoba mosi 2018. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Kifua Kikuu, Ulinzi wa Amani, tukio maalum la kumuenzi hayati Nelson Mandela na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, NCDs.
MKUTANO WA 73 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Marufuku ya plastiki za kutumia na kutupa UN ni moja ya mafanikio yangu- Maria Espinosa
Rais wa mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaotamatishwa hii leo, María Fernanda Espinosa ametaja marufuku ya plastiki zinazotumiwa mara moja na kutupwa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani kuwa moja ya mafanikio makubwa ya kipindi chake.
Tuhakikishe watu ni msingi wa kila jambo tunalofanya 2019- Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaja maeneo matatu ya utekelezaji kwa mwaka huu wa 2019.
Espinosa ataja vipaumbele vyake mkutano 73 ukibakiza miezi 8
Ikiwa imesalia miezi nane kabla ya kumalizika kwa mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, hii leo Rais wa baraza hilo, Maria Fernanda Espinosa amezungumza na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa na kueleza vipaumbele saba atakavyozingatia wakati wa kipindi hicho.
Ukatili dhidi ya wanawake Uganda sio majumbani tu hata vyuoni
Tatizo la ukatili wa kijinsia ni kubwa duniani kote ndio maana Umoja wa Mataifa umelivalia njuga ili kuhakikisha ukatili huo unakomeshwa, lakini pia lengo namba 5 la maendeleo endelevu yaani SDG’s lihusulo usawa wa kijinsia linatimia ifikapo 2030.
Mjadala Mkuu wa #UNGA73 wafunga pazia, Lithuania yavunja rekodi kwa hotuba fupi zaidi
Waliohutubia UNGA73: Marais 77, wakuu 44 wa serikali, mawaziri 54, naibu mawaziri wakuu 4, Naibu Waziri 1, wawakilishi 8 wa kudumu wa nchi kwenye Umoja wa Mataifa.
Sasa kuna nuru kwa Sudan na Sudan Kusini kumaliza tofauti zao- Waziri Eldirdiri
Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan, Mohamed Ahmed Eldirdiri amehutubia mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kusema kuwa mazingira ya sasa yanatia moyo katika kupatia suluhu masuala yote yaliyosalia kati ya nchi yake na Sudan Kusini.
Vijana mamlakani leo, ni wazee kesho! Pangeni mustakabali mnaotaka-Mtaalamu
Wakati kukishuhudiwa mabadiliko ya hali ya jamii, mchango wa wazee katika kuchagiza haki za binadamu ni muhimu sasa kuliko wakati mwingine.
Chonde chonde Umoja wa Mataifa tuondoleeni vikwazo vya silaha:Somalia
Ninausihi Umoja wa Mataifa kuiondolea Somalia vikwazo vya ununuzi wa silaha . Wito huo umetolewa leo na Ahmed Isse Awad Waziri wa mambo ya nje wa Somalia akihutubia mjadala wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kikao cha 73 mjini New York Marekani hii leo.
Wanahabari 262 wamefungwa mwaka jana pekee, hii si haki:UN
Waandishi wa mara kwa mara hutishwa, hushambuliwa na hata kuuawa, na idadi kubwa wanafungwa gerezani duniani kote. Hayo yameelezwa bayana na wataalamu wa haki za binadamu kwenye mkutano uliofanyika kandoni mwa mjadala wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaoendelea mjini New York Marekani.
Sasa Burundi tuna amani na wakimbizi wanarejea nyumbani:Nibigira
Waziri wa mambo ya nje wa Burundi Ezechiel Nibigira ameuambia mjadala wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kikao cha 73 unaoendelea mjini New York Marekani kuwa hivi sasa taifa lake lina utulivu na amani na wakimbizi walioko nje wameanza kurejea nyumbani, hivyo ni wakati wa Baraza la Usalama kuacha kulijadili taifa hilo kila uchao.