Yemen: Badala ya kununua sabuni sasa nanunua chakula, asante UNICEF
Huduma za kujisafi na usafi mara nyingi husalia ndoto kwa wakimbizi wa ndani kwa kuwa kipaumbele kinakuwa ni usalama wao hali inayoongeza zaidi hatari ya kupata magonjwa iwapo wanakosa huduma hizo na ndio maana nchini Yemen, Umoja wa Mataifa umechukua hatua kuwezesha wayemen waishio kambini wanaweza kujikinga pia na magonjwa yatonayo na uchafu.