Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA

MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
MJADALA MKUU WA UNGA74

Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 22 septemba 2019 hadi 30 Septemba 2019. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu  Mkutano wa vijana wa vijana na mabadiliko ya tabianchi, fursa ya afya kwa wote, mkutano kuhusu fursa ya afya kwa wote, tathimini ya hatua za utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, ufadhili kwa ajili ya maendeleo na tathimini ya mwelekeo wa mkakati wa SAMOA.

UN/Cia Pak

Elimu, ujumuishwaji na mabadiliko ya tabianchi ni baadhi vya vipaumbele vya Kenya aeleza Rais Uhuru Kenyatta

Tumefika hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kuungana na nchi wanachama kuelezea ambayo Kenya imeyafanya katika kuhakikisha inaendana na vipaumbele vya mkutano huu wa Baraza Kuu la Umoja huo UNGA74 ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, ujumuishwaji na ushirikiano wa kuhakisha utimizaji wa malengo ya maendeleo endelevu SDGs ifikapo mwaka 2030.

Sauti
2'4"
Félix Antoine Tshilombo Tshisekedi, rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC wakati wa hotuba yake kwa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74
UN Photo/Cia Pak

Dunia inahitaji madini,  ajira za viwandani, mafunzo na maendeleo- rais Tshisekedi

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC inauhitaji Ujumube wa Umoja wa Mataifa nchini DRC, MONUSCO lakini inahitaji MONUSCO iliyo haraka kutekeleza wajibu wake, ulio na vifaa, ulio  thabiti na ambao una wajibu sahihi, amesema rais wa DRC, Felix Tshisekedi katika hotuba yake ya kwanza kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Leo Alhamisi Septemba 26.