Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 22 septemba 2019 hadi 30 Septemba 2019. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Mkutano wa vijana wa vijana na mabadiliko ya tabianchi, fursa ya afya kwa wote, mkutano kuhusu fursa ya afya kwa wote, tathimini ya hatua za utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, ufadhili kwa ajili ya maendeleo na tathimini ya mwelekeo wa mkakati wa SAMOA.
MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Kenya tunasonga ingawa bado tuko mbali, asema Rais Uhuru Kenyatta
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema nchi yake inajitahidi katika utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu na imepiga hatua ingawa bado kuna safari ndefu.
Teknolojia mpya zina hatari kubwa:Boris Johnson
Teknolojia mpya zina hatari kubwa, ameonya waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson akihutubia Jumanne usiku mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaoendelea kwenye makao makuu ya Umoja huo jijini New York Marekani.
26 Septemba 2019
Wanawake wanahitajika zaidi katika tasnia ya ubaharia kama ilivyo tasnia nyingine, linasema shirika la kimataifa la shughuli za usafirishaji wa majini IMO. Elimu, ujumuishwaji na mabadiliko ya tabianchi ni baadhi vya vipaumbele vya Kenya asema Rais Uhuru Kenyatta. Na Profesa Antoine Kiamiantako Miyamueni, mdadhiri wa masuala ya uchumi katika chuo kikuu cha Kinshasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ( DRC) amesema ushirikiano baina ya vyuo vikuu utasaidia kuinua elimu Afrika.
Ushirikiano baina ya vyuo vikuu utasaidia kuinua elimu Afrika- Profesa Miyamueni
Jukwaa la kimataifa la vyuo vikuu barani Afrika na ughaibuni kuhusu malengo ya maendeleo endelevu na mustakabali wa elimu katika bara hilo, limezinduliwa rasmi kwenye makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani.
Elimu, ujumuishwaji na mabadiliko ya tabianchi ni baadhi vya vipaumbele vya Kenya:rais Kenyatta
Tumefika hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kuungana na nchi wanachama kuelezea ambayo Kenya imeyafanya katika kuhakikisha inaendana na vipaumbele vya mkutano huu wa Baraza Kuu la Umoja huo UNGA74 ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, ujumuishwaji na ushirikiano wa kuhakisha utimizaji wa malengo ya maendeleo endelevu SDGs ifikapo mwaka 2030.
‘Mkono kwa mkono’ kunusuru njaa katika nchi maskini- FAO
Shirika la chakula na kilimo duniani, FAO limesema kitendo cha nchi wanachama wa Umoja waMataifa kusaidia na kuunga mkono harakati za shirika hilo kama mpango mpya wa Mkono kwa Mkono, kitaasaidia kuchagiza mafanikio ya malengo ya maendeleo endelevu, SDGs hususan lile la kutokomeza njaa, na hivyo kutomwacha nyuma mtu yeyote.
Kenya tunasonga ingawa bado tuko mbali-Kenyatta
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema nchi yake inajitahidi katika utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu na imepiga hatua ingawa bado kuna safari ndefu.
Ahadi ni deni: Mkutano wa kihistoria kutoa msukumo wa ufadhili kwa ajili ya maendeleo.
Umoja wa Mataifa unasema uchumi endelevu wa dunia ule ambao unailinda dunia na kuboresha maisha ya kila mtu kila mahali ni fursa nzuri ya kuleta ajira na masoko yenye thamani ya matrilioni ya dola. Ili kutimiza hilo , jamii ya kimataifa inahitaji kuongeza kasi ya uwekezaji.
Tunaomba jamii ya kimataifa kwenda nasi bega kwa bega kutatua majanga CAR - rais Touadera
Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, Faustin Archange Touadera hii leo Jumatano ametoa wito wa ushirikiano wa kimataifa, tofauti, unaoeleweka, na ulio na utaratibu katika kukabiliana na janga linalokabili nchi yake, akielezea msaada wa serikali kuendelea kusaidia raia wake kuibuka kutoka hali ya sasa.
Licha ya hatua zilizopigwa, safari bado ni ndefu kutimiza haki za mtoto- Katibu Mkuu
Tangu kupitishwa kwa mkataba wa haki za mtoto miaka 30 iliyopita pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana kote duniani bado vita imesalia kuwa chanzo kubwa ya ukiukwaji wa haki za mtoto na bado kuna nchi hazijaridhia mkataba huo amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.