Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA

MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
MJADALA MKUU WA UNGA74

Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 22 septemba 2019 hadi 30 Septemba 2019. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu  Mkutano wa vijana wa vijana na mabadiliko ya tabianchi, fursa ya afya kwa wote, mkutano kuhusu fursa ya afya kwa wote, tathimini ya hatua za utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, ufadhili kwa ajili ya maendeleo na tathimini ya mwelekeo wa mkakati wa SAMOA.

Himaya ya vijana kwenye Makao makuu ya Umoja wa Mataifa
UN Photo/Laura Jarriel

Habari njema ni kwamba ajenda ya 2030 sasa inahuishwa japo kibarua bado kipo:Guterres

Safari ya malengo ya maendeleo endelevu au SDGs alianza mwaka 2015 na kila mtu anajua wapi ni mwisho wa safari yetu, kutokomeza umasikini na njaa, usawa kwa wanawake na wasichana , kuwawezesha vijana, kupunguza hewa ukaa, kuwa na uchumi wa kukabili mabadiliko ya tabianchi, ajira zenye hadi na mafanikio ya pamoja, jamii zenye amani na haki, haki za binadamu kwa wote na kuheshimu utawala wa sheria. Pia fursa kwa wote za kuishi katika dunia bora.

24 Septemba 2019

Hofu imegeuzwa mtaji hivi sasa duniani, Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres aueleza mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74. Waziri wa afya wa Kenya Sicily Kariuki asema ili tutimize SDGs Kenya lazima tuhakikishe huduma za afya kwa wote.  Naye Waziri wa fedha na mipango wa Tanzania Dkt Philip Mpango atoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kushirikiana kutekeleza SDGs.

Sauti
14'2"