Kwa takribani miongo mitatu, Umoja wa Mataifa (UN) umekuwa ukileta pamoja kila nchi duniani kwenye mikutano ya ngazi ya juu kuhusu tabianchi, mikutano ikipatiwa jina COP yaani conference of Parties kwa kiswahli wanachama wa mkutano. Tangu wakati huo, mabadiliko ya tabianchi yamebadilika kutoka suala la pembezoni hadi kipaumbele cha kimataifa.
Mwaka huu utakuwa mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mikutano hiyo, ikipatiwa jina COP26. Uingereza ndio Rais wa mkutano hou wa COP26 na unafanyika Glasgow, Scotland.
Kuelekea COP26, Uingereza inafanya kazi na kila taifa kufikia makubaliano ya jinsi ya kukabili mabadiliko ya tabianchi. Viongozi wa dunia wanawasili Scotland, sambamba na makumi ya maelfu ya washauri, wawakilishi wa serikali, sekta ya biashara, wananchi kwa ajili ya mkutano huo wa siku 12.
Si tu kwamba ni jukumu kubwa, bali pia ni tofaauti na mikutano mingine iliyotangulia ya nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi. Wataalamu wengi wanaamini kuwa COP26 ni dharura ya kipekee.
Ili kupokea taarifa za kila wakati moja moja kwenye akaunti yako ya barua pepe, tafadhali hakikisha unajisajili hapa kwenye mada kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi
COP26
Madhara ya tabianchi yanachanja mbuga, hatua kwa tabianchi zinadorora- UN
Wawakilishi wa serikali wakianza kukamilisha ajenda kwa ajili ya mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP27 utakaofanyika mwezi ujao huko Misri, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewaambia waandishi wa habari jijini New York, Marekani kuwa kazi iliyo mbele ni kubwa na nzito wakati huu ambapo madhara ya tabianchi yanashuhudia kote duniani.
Mabadiliko ya tabiachi yaanza kubadilisha maisha ya jamii ya Maasai, Loliondo, Tanzania
Watu jamii ya Maasai huko Loliondo, wilaya ya Ngorongo, Tanzania ambao kwa miaka yote ya uwepo wao shuguli yao ya kujipatia kipato na chakula ni kupitia mifugo hususani ng’ombe, na chakula chao ni nyama na maziwa, sasa wameanza kulazimika kuanza kuhamia katika shughuli za kilimo baada ya shughuli yao hiyo ya asili ufugaji kuathiriwa na mabadiliko ya tabianchi.
31 DESEMBA 2021
Katika jarida la matukio ya mwaka la Umoja wa Mataifa hii leo Assumpta Massoi anakuletea
-Wanajeshi watatu wa kulinda amani kutoka Tanzania wanaohudumu kwenye mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati MINUSCA, wamejeruhiwa na mmoja vibaya sana baada ya msafara wao kukanyaga vilipuzi. Wote wanatibiwa hospitalini mjini Bangui
-Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema mwaka huu umekuwa wa machungu na ukiukwaji mkubwa wa haki za watoto katika mizozo ya muda mrefu na ile mipya.
Ili kutimiza lengo la mabadiliko ya tabianchi lazima tutimize lengo la misitu:FAO/UNECE
Athari za mabadiliko ya tabia nchi kwenye misitu zitakuwa kubwa imesema ripoti iliyotolewa leo na shirikia la Umoja wa Mataifa la chakula na Kilimo FAO kwakushirikinana na kamisheni ya masuala ya uchumi barani ulaya UNECE.
Hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi zinaweza kukuza utu, fursa na usawa: Mohammed
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed ameshiriki katika majadiliano ya TED yanayosisitiza fursa za kuondokana na mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi kwa kuchangisha fedha zaidi na mshikamano, wakati huu ambao "fursa bado ipo".
COP26 inafunga kwa makubaliano ya ‘maelewano’ lakini haitoshi, asema Mkuu wa Umoja wa Mataifa
Baada ya kongeza siku moja ya mazungumzo ya mabadiliko ya tabianchi ya COP26, karibu nchi 200 huko Glasgow, Scotland, zimepitisha hati ya matokeo hii leo hati ambayo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, amesema inaangazia masilahi ya pamoja, kinzani, na hali ya dhamira ya kisiasa ulimwenguni leo.
12 Novemba 2021
Karibu kusikiliza jarida ambapo leo Mada yetu kwakina inatokea huko Glasgow Scotland ambapo mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi COP26 ukiwa unafunga pazia mwanaharakati wa Mazingira Dkt. Sixbert Mwanga kutoka nchini Tanzania anasema Afrika pamoja na kuwa na kauli moja lakini haijafanikiwa kwenye mkutano huo.
Pia utasikia habari kwa ufupi na kupata fursa ya kujifunza kiswahili .
Afrika haijafanikiwa kwenye mkutano wa COP26: Dkt. Sixbert Mwanga
Mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi COP26 unafunga pazia huko Glasgow Scotland ambapo mwanaharakati wa Mazingira Dkt. Sixbert Mwanga kutoka nchini Tanzania anasema Afrika pamoja na kuwa na kauli moja lakini haijafanikiwa kwenye mkutano huo.
Wakati umefika kugeukia usafiri unaolinda mazingira: COP26
Kuwa na dunia ambayo vyombo vya usafiri kama magari, mabasi na malori ambayo yanatumia umeme n ani ya gharama nafuu, kuwa dunia ambayo vyombo wa usafiri wa bahari vinatumia nishati safi pekee na ndege ziweze kusafiri kwa kutumia hewa safi ya Hydrogen inaweza kuonekana kama ndoto ama sinema lakini kwenye mkutano wa COP26 unaoendelea huko Glasgow serikali nyingi na makampuni ya biashara wamesema wameanza kutimiza ndoto hizi na kuzifanya kuwa hali halisi.
Ahadi ni hewa iwapo miradi ya makaa ya mawe na mafuta ya kisukuku inaendelea kupatiwa fedha- Guterres
Mkutano wa COP26 ukifikia ukingoni huko Glasgow, Scotland, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amezisihi serikali zioneshe hatua nyingi zaidi za kukabili, kuhimili na kufadhili miradi ya tabianchi kwa njia bora zaidi iwapo haziwezi kufikia kiwango cha chini zaidi kilichowekwa.