Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

COP26

COP26: 31 Oktoba-12 Novemba 2021 | Glasgow, Uingereza

Kwa takribani miongo mitatu, Umoja wa Mataifa (UN) umekuwa ukileta pamoja kila nchi duniani kwenye mikutano ya ngazi ya juu kuhusu tabianchi, mikutano ikipatiwa jina COP yaani conference of Parties kwa kiswahli wanachama wa mkutano. Tangu wakati huo, mabadiliko ya tabianchi yamebadilika kutoka suala la  pembezoni hadi kipaumbele cha kimataifa.
 
Mwaka huu utakuwa mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mikutano hiyo, ikipatiwa jina COP26. Uingereza ndio Rais wa mkutano hou wa COP26 na unafanyika Glasgow, Scotland.
Kuelekea COP26, Uingereza inafanya kazi na kila taifa kufikia makubaliano ya jinsi ya kukabili mabadiliko ya tabianchi. Viongozi wa dunia wanawasili Scotland, sambamba na makumi ya maelfu ya washauri, wawakilishi wa serikali, sekta ya biashara, wananchi kwa ajili ya mkutano huo wa siku 12.
Si tu kwamba ni jukumu kubwa, bali pia ni tofaauti na mikutano mingine iliyotangulia ya nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi. Wataalamu wengi wanaamini kuwa COP26 ni dharura ya kipekee.
Ili kupokea taarifa za kila wakati moja moja kwenye akaunti yako ya barua pepe, tafadhali hakikisha  unajisajili hapa kwenye mada kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi

Senegal ni moja kati ya nchi 6 zilizoathirika na ukame mkali mwaka huu
UNOCHA/Eve Sabbagh

Ukweli ulio wazi ni kwamba dunia inaelekea kwenye zahma ya mabadiliko ya tabianchi:Guterres

Tuko katika wakati muhimu kwa sayari yetu. Lakini wacha tuwe wazi  kuna hatari kubwa ambayo mkutano wa mabadiliko ya tabianchi wa Glasgow unaweza usizai matunda, ameonya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo akizungumza na waandishi wa Habari mjini Roma Italia kunakofanyika mkutano wa mataifa 20 yaliyoendelea kiuchumi duniani au G-20.

29 Oktoba 2021

Karibu kusikiliza jarida ambapo kama ilivyo ada ijumaa tunakuletea mada kwa kina leo tukimulika usanifu majengo na udhibiti wa mabadiliko ya tabianchi mijini kuelekea siku ya miji duniani tarehe 31 mwezi huu wa Oktoba.

Pia utasikia habari kwa ufupi zikiangazia wito uliotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya hewa duniani na mashirika mengine ya kimataifa tisa kuhusu maji na mabadiliko ya tabianchi. Taarrifa nyingine ni Maendeleo ya teknolojia kwa wanahabari na asasi za kiraia pamoja na mbinu bora na za kimkakati za kuwalinda watoto walioathiriwa na migogoro

Sauti
17'41"
Mtoto akiwa juu ya lundo la mchanga ambao hutumiwa na wakazi wa eneo hili kujaribu kuzuia maji ya ziwa Albert yasiingie kwenye makazi yao.
UN/ John Kibego

Jipime ufahamu wako kuhusu COP26

Mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP26 unafanyika Glasgow, Scotland. Je unafahamu kwa kiwango gani yanayojadili? Hapa kuna fursa ya kujaribu uelewa wako kupitia maswali yetu kwako kuhusu mabadiliko ya tabianchi. (Majibu yako chini kabisa ya ukurasa huu) 

Naibu Katibu Mkuu wa UN Amina J. Mohammed (kati) na Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbambwe pamoja na washiriki wengine wa mkutaon wa kikanda wa Afrika kuhusu maendeleo endelevu, mkutano uliofanyika Zimbabawe.
ECA

Kuelekea mkutano wa tabiachi, jipambanue na vifupisho vya misamiati yake

Kama umekuwa unafuatiliwa Umoja wa Mataifa au UN kwa muda mrefu, bila shaka utakuwa umeshuhudia mlolongo wa vifupisho vya maneno na misamiati migumu ambayo ni nadra kuleta maana kwa msomaji asiyehusika na Nyanja husika. Hii huleta mkanganyiko na hata wakati mwingine mtu kushindwa kufuatilia Habari husika. Tunapoelekea mkutano wa tabianchi huko Glasglow,  Scotland tunaona ni bora kuchambua vifupisho hivyo ili uweze kunufaika na mkutano huo sambamba na taarifa za taifa lako.  

Jarida 30 Septemba 2021

Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya sekta ya bahari , janga la corona au COVID-19 limethibitisha umuhimu wa bahari na kujitolea kwa mamilioni ya mabaharia wanaofanyakazi katika sekta hiyo amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.

Karibu usikilize jarida linaloletwa kwako na Assumpta Massoi ambapo atakujuza kwa undani taarifa hiyo na nyingine nyingi.

Sauti
12'14"