Kwa takribani miongo mitatu, Umoja wa Mataifa (UN) umekuwa ukileta pamoja kila nchi duniani kwenye mikutano ya ngazi ya juu kuhusu tabianchi, mikutano ikipatiwa jina COP yaani conference of Parties kwa kiswahli wanachama wa mkutano. Tangu wakati huo, mabadiliko ya tabianchi yamebadilika kutoka suala la pembezoni hadi kipaumbele cha kimataifa.
Mwaka huu utakuwa mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mikutano hiyo, ikipatiwa jina COP26. Uingereza ndio Rais wa mkutano hou wa COP26 na unafanyika Glasgow, Scotland.
Kuelekea COP26, Uingereza inafanya kazi na kila taifa kufikia makubaliano ya jinsi ya kukabili mabadiliko ya tabianchi. Viongozi wa dunia wanawasili Scotland, sambamba na makumi ya maelfu ya washauri, wawakilishi wa serikali, sekta ya biashara, wananchi kwa ajili ya mkutano huo wa siku 12.
Si tu kwamba ni jukumu kubwa, bali pia ni tofaauti na mikutano mingine iliyotangulia ya nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi. Wataalamu wengi wanaamini kuwa COP26 ni dharura ya kipekee.
Ili kupokea taarifa za kila wakati moja moja kwenye akaunti yako ya barua pepe, tafadhali hakikisha unajisajili hapa kwenye mada kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi
COP26
Ukweli ulio wazi ni kwamba dunia inaelekea kwenye zahma ya mabadiliko ya tabianchi:Guterres
Tuko katika wakati muhimu kwa sayari yetu. Lakini wacha tuwe wazi kuna hatari kubwa ambayo mkutano wa mabadiliko ya tabianchi wa Glasgow unaweza usizai matunda, ameonya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo akizungumza na waandishi wa Habari mjini Roma Italia kunakofanyika mkutano wa mataifa 20 yaliyoendelea kiuchumi duniani au G-20.
Usanifu majengo ni msingi wa mnepo wa majengo mijini
Tarehe 31 ya mwezi Oktoba kila mwaka ni siku ya majiji na miji duniani ambapo kwa mwaka huu maudhui ni Kuwezesha miji kuwa na mnepo kwa tabianchi. Maudhui haya yamekuja wakati ambapo miji inapaswa kuwa na mnepo kuliko wakati wowote ule.
Ni wakati wa kuchukua hatua haraka kwa ajili ya maji na mabadiliko ya tabianchi
Mkuu wa shirika la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO na mashirika mengine tisa ya kimataifa yametoa wito wa pamoja na wa dharura kwa serikali kuweka kipaumbele kwa hatua jumuishi za maji na mabadiliko ya tabianchi kutokana na athari zinazoenea za masuala hayo kwa maendeleo endelevu.
29 Oktoba 2021
Karibu kusikiliza jarida ambapo kama ilivyo ada ijumaa tunakuletea mada kwa kina leo tukimulika usanifu majengo na udhibiti wa mabadiliko ya tabianchi mijini kuelekea siku ya miji duniani tarehe 31 mwezi huu wa Oktoba.
Pia utasikia habari kwa ufupi zikiangazia wito uliotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya hewa duniani na mashirika mengine ya kimataifa tisa kuhusu maji na mabadiliko ya tabianchi. Taarrifa nyingine ni Maendeleo ya teknolojia kwa wanahabari na asasi za kiraia pamoja na mbinu bora na za kimkakati za kuwalinda watoto walioathiriwa na migogoro
Jipime ufahamu wako kuhusu COP26
Mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP26 unafanyika Glasgow, Scotland. Je unafahamu kwa kiwango gani yanayojadili? Hapa kuna fursa ya kujaribu uelewa wako kupitia maswali yetu kwako kuhusu mabadiliko ya tabianchi. (Majibu yako chini kabisa ya ukurasa huu)
Mnyama aliyetoweka mamilioni ya miaka atumika kuwakumbusha wanadamu kutochagua kutoweka
Mnyama aliyetoweka mamilioni ya miaka atumika kuwakumbusha wanadamu kutochagua kutoweka (OVERNIGHT)
Dunia ikiwa inaelekea katika mkutano wa tabianchi huko Glasgow, Scotland, Umoja wa Mataifa umemtumia "shuhuda" asiye wa kawaida kueleza hatari zinazoukabili ulimwengu ikiwa mienendo ya binadamu wa sasa ya kuharibu mazingira haitabadilika.
Kuelekea mkutano wa tabiachi, jipambanue na vifupisho vya misamiati yake
Kama umekuwa unafuatiliwa Umoja wa Mataifa au UN kwa muda mrefu, bila shaka utakuwa umeshuhudia mlolongo wa vifupisho vya maneno na misamiati migumu ambayo ni nadra kuleta maana kwa msomaji asiyehusika na Nyanja husika. Hii huleta mkanganyiko na hata wakati mwingine mtu kushindwa kufuatilia Habari husika. Tunapoelekea mkutano wa tabianchi huko Glasglow, Scotland tunaona ni bora kuchambua vifupisho hivyo ili uweze kunufaika na mkutano huo sambamba na taarifa za taifa lako.
Tukifanya kazi pamoja tunaweza kukabili changamoto za mabadiliko ya tabianchi:UN
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo limekutana katika mjadala wa wazi kujadili mabadiliko ya tabianchi ukijikita na mada “Utekelezaji wa hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kwa ajili ya watu, sayari dunia na ustawi.”
Jarida 30 Septemba 2021
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya sekta ya bahari , janga la corona au COVID-19 limethibitisha umuhimu wa bahari na kujitolea kwa mamilioni ya mabaharia wanaofanyakazi katika sekta hiyo amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.
Karibu usikilize jarida linaloletwa kwako na Assumpta Massoi ambapo atakujuza kwa undani taarifa hiyo na nyingine nyingi.
Mwanya wa kuepuka zahma ya mabadiliko ya tabianchi unaziba haraka:Guterres
Hakuna eneo ambalo lina kinga dhidi ya majanga ya mabadiliko ya tabianchi Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameliambia Baraza la Usalama leo Alhamisi, akionya kuwa "fursa yetu ya kuzuia athari mbaya zaidi za mabadiliko ya tabianchi inafunga haraka".