Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

COP26

COP26: 31 Oktoba-12 Novemba 2021 | Glasgow, Uingereza

Kwa takribani miongo mitatu, Umoja wa Mataifa (UN) umekuwa ukileta pamoja kila nchi duniani kwenye mikutano ya ngazi ya juu kuhusu tabianchi, mikutano ikipatiwa jina COP yaani conference of Parties kwa kiswahli wanachama wa mkutano. Tangu wakati huo, mabadiliko ya tabianchi yamebadilika kutoka suala la  pembezoni hadi kipaumbele cha kimataifa.
 
Mwaka huu utakuwa mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mikutano hiyo, ikipatiwa jina COP26. Uingereza ndio Rais wa mkutano hou wa COP26 na unafanyika Glasgow, Scotland.
Kuelekea COP26, Uingereza inafanya kazi na kila taifa kufikia makubaliano ya jinsi ya kukabili mabadiliko ya tabianchi. Viongozi wa dunia wanawasili Scotland, sambamba na makumi ya maelfu ya washauri, wawakilishi wa serikali, sekta ya biashara, wananchi kwa ajili ya mkutano huo wa siku 12.
Si tu kwamba ni jukumu kubwa, bali pia ni tofaauti na mikutano mingine iliyotangulia ya nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi. Wataalamu wengi wanaamini kuwa COP26 ni dharura ya kipekee.
Ili kupokea taarifa za kila wakati moja moja kwenye akaunti yako ya barua pepe, tafadhali hakikisha  unajisajili hapa kwenye mada kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi

Chama cha ushirika cha wanawake kusini mwa Mauritania kinatumia nishati ya sola kuendesha mtambo wa kumwagilia maji kwenye bustani za mboga.
Climate Visuals Countdown/Raphael Pouget

COP26: Hakuna tena maneno matupu, sekta binafsi zajitoa kimasomaso- Carney

Katika siku inayomulika sekta ya fedha na udhibiti wa mabadiliko ya tabianchi kwenye mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mabadiliko ya tabianchi, COP26 huko Glasgow, Scotland, takribani kampuni binafsi 500 zimekubaliana kutenga dola trilioni 130 kutekeleza mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi ikiwemo hakikisha kiwango cha joto duniani hakizidi nyuzijoto 1.5  katika kipimdo cha Selsiyasi. 

3 Novemba 2021

Karibu katika jarida ambapo utasikia kuhusu ushindi wa kijana mtanzania katika tuzo zilizotolewa leo sanjari na mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP26.

Habari kwa ufupi leo zimeangazia ripoti ya uchuguzi wa masuala ya haki za binadamu huko Tigray nchini Ethiopia na baa la njaa nchiniMadagascar

Sauti
13'14"