Kwa takribani miongo mitatu, Umoja wa Mataifa (UN) umekuwa ukileta pamoja kila nchi duniani kwenye mikutano ya ngazi ya juu kuhusu tabianchi, mikutano ikipatiwa jina COP yaani conference of Parties kwa kiswahli wanachama wa mkutano. Tangu wakati huo, mabadiliko ya tabianchi yamebadilika kutoka suala la pembezoni hadi kipaumbele cha kimataifa.
Mwaka huu utakuwa mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mikutano hiyo, ikipatiwa jina COP26. Uingereza ndio Rais wa mkutano hou wa COP26 na unafanyika Glasgow, Scotland.
Kuelekea COP26, Uingereza inafanya kazi na kila taifa kufikia makubaliano ya jinsi ya kukabili mabadiliko ya tabianchi. Viongozi wa dunia wanawasili Scotland, sambamba na makumi ya maelfu ya washauri, wawakilishi wa serikali, sekta ya biashara, wananchi kwa ajili ya mkutano huo wa siku 12.
Si tu kwamba ni jukumu kubwa, bali pia ni tofaauti na mikutano mingine iliyotangulia ya nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi. Wataalamu wengi wanaamini kuwa COP26 ni dharura ya kipekee.
Ili kupokea taarifa za kila wakati moja moja kwenye akaunti yako ya barua pepe, tafadhali hakikisha unajisajili hapa kwenye mada kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi
COP26
Mjadala Mkuu wa UNGA76 wafungua pazia New York
Mjadala Mkuu wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA76 leo umeng’oa nanga rasmi katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa hapa jijini New York Marekani ukifanyika moja kwa moja na pia kupitia mtandaoni ukiwaleta pamoja nchi 193 wanachama wa Umoja huo.
Flora Nducha na taarifa zaidi
Abdullah Shahid Rais wa Baraza Kuu akifungua mjadala huo ambao umebeba mada ya “Kujenga mnepo kupitia tumaini la kujikwamua kutoka kwa janga la COVID-19, kushughulikia mahitaji ya sayari dunia, kuheshimu haki za watu, na kuufufua Umoja wa Mataifa. "
Mjadala Mkuu wa ngazi za juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa waanza rasmi
Mjadala Mkuu wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA76 leo umeng’oa nanga rasmi katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa hapa jijini New York Marekani ukifanyika moja kwa moja na pia kupitia mtandaoni ukiwaleta pamoja nchi 193 wanachama wa Umoja huo.
Hatupaswi kukata tamaa, tuna nia ya kujinasua kutimiza SDGs:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameiasa dunia kutopoteza matumaini hata kama mambo yanakwenda kombo katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu SDGs ili kutimiza lengo ifikapo mwaka 2030.
Muda unatutupa mkono kuepuka janga la mabadiliko ya tabianchi:UN Ripoti
Kupunguzwa kwa muda kwa uzalishaji wa hewa ukaa kulikosababishwa na masharti ya kimataifa ya watu kusalia majumbani wakati wa janga la corona au COVID-19 hakukupunguza kasi ya kuendelea kwa mabadiliko ya tabianchi. Viwango vya gesi chafuzi vimevunja rekodi, na dunia iko njiani kuelekea hatari joto kali la kupindukia, imeonya ripoti ya mabadiliko ya tabia nchi iliyotolewa leo na mashirika mbalimbali.
Naibu Katibu Mkuu wa UN na serikali ya Kenya wajadili ushirikiano, COVID-19 na usalama
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed yuko ziarani Afrika Mashariki ambapo akiwa nchini Kenya amepata fursa ya kuzungumza na viongozi wa serikali ya nchi hiyo.
Hakuna njia ya kufikia Mkataba wa Paris wa lengo la nyuzi joto 1.5˚C bila G20 – Katibu Mkuu UN
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo Jumapili amesema, "Ulimwengu unahitaji haraka kujitolea kwa mataifa yote ya G20 kuliko wazi na kusiko na utata kwenye lengo la nyuzi joto 1.5 za selisiasi la Mkataba wa Paris.”
Chanjo zinapaswa kuzingatiwa kama "bidhaa za umma ulimwenguni" - Guterres
Akiongea kupitia video huko London, Uingereza, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema hakuna njia nyingine ya kushinda virusi vinavyoenea katika nchi zinazoendelea "kama moto wa nyikani" na hatari za kubadilika, isipokuwa kwa njia ya usawa, chanjo kwa watu wengi, na kuongeza kuwa chanjo zinahitajika "kupatikana na za bei nafuu kwa wote ”
Maneno matupu hayavunji mfupa, ni wakati wa vitendo dhidi ya mabadiliko ya tabianchi:UN
Nchi zinazowakilisha asilimia 70 ya uchumi wa dunia na wachangiaji wa asilimia 65 ya hewa ukaa sasa zimeahidi ushiriki wao katika kutokomeza kabisa hewa ukaa.
Guterres amteua tena Bloomberg kuwa mjumbe wake maalum wa tabianchi
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amemteua tena Michael Bloomberg wa Marekani kuwa mjumbe wake maalum wa hatua thabiti na zenye matamanio makubwa katika kukabili tabianchi.
COVID-19 ni somo kwamba, hatuwezi kumudu kupuuza hatari tunazozifahamu :Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema janga la Corona au COVID-19 ni somo tosha la kukumbusha kwamba dunia haiwezi kumudu kupuuza hatari inazozijua.