UNICEF Rwanda: Programu ya “Winsiga Ndumva” waleta zawadi ya sauti kwa watoto viziwi
Kupitia mradi wa "Winsiga Ndumva", maneno ya lugha ya Kinyarwanda yanayomaanisha "Usiniache nyuma, ninaweza kusikia”, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na wadau wake ikiwemo Wizara ya Afya nchini Rwanda limebadilisha maisha ya watoto wengi na vijana ambao walikuwa na changamoto ya masikio na kuongea kwakuwapatia vifaa maalumu vya kupachika masikioni ili kusaidia masikio kufanya kazi yake ipasavyo.