WFP yasaidia raia zaidi ya milioni moja kaskazini mashariki mwa Nigeria
Shirika la mpango wa chakula duniani WFP limesema kuwa tangu mwanzo wa mwezi huu wa Desemba, limetoa msaada wa chakula au fedha kwa zaidi ya raia milioni moja katika maeneo yenye vita kwa walioathirika katika Kaskazini mashariki mwa Nigeria. Hii inamaanisha kwamba zaidi ya nusu ya wale wanaohitaji msaada wa kibinadamu kwa haraka sasa wamefikiwa.
Hatua hii inakuja wakati shirika hilo linawasaidia raia katika majimbo ya Borno na Yobe nchini Nigeria ambako takriban watu milioni nne wana uhaba wa chakula.