Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Photo: OCHA Burundi / Ana Maria Pereira

Nchini Burundi mbinu ya mashangazi na baba wa shuleni yaepusha watoto na kejeli kutoka kwa wenzao

Nchini Burundi shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limechukua hatua kuhakikisha watoto wakimbizi wanaorejea nchini humo wanaweza kuendelea na elimu bila uoga na jakamoyo hasa pale wanapokumbana na vizuizi vya tofauti ya lugha waliyotumia ukimbizini na ile inayotumika nyumbani walikorejea. 

Hebu fikiria baada ya machungu ya ukimbizini, unarejea nyumbani nako shuleni unakumbwa na kejeli kisa tu matamshi ya lugha utumiayo ni tofauti na yale ya wenzako darasani. 

Sauti
2'21"
© FAO/Luis Tato

Kaveh Zahedi wa FAO: Hatuwezi kuwa tu watazamaji wa mabadiliko ya tabianchi, kilimo kina jukumu

Kilimo kinaweza kuchukua jukumu kuu katika hatua dhidi ya tabianchi wakati huo huo kikihakikisha uhakika wa chakula duniani, ni maoni ya Mkurugenzi wa Ofisi ya Mabadiliko ya Tabianchi, Bayonuai na Mazingira katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) Kaveh Zahedi kufuatia hivi majuzi mwaka 2023 kuthibitishwa kuwa mwaka wa joto zaidi katika rekodi za dunia. 

Audio Duration
1'18"
© UNICEF/Eyad El Baba

UN yaomba kufunguliwe njia nyingine ya kufikisha misaada Gaza

Zikiwa ni zaidi ya siku 100 tangu kuibuka upya kwa mzozo huko Mashariki ya Kati, mashirika ya Umoja wa Mataifa hii leo wametoa taarifa inayoeleza kuongezeka kwa hatari ya baa la njaa na milipuko ya magonjwa ya kuambukiza huku yakisisitiza muarobaini pekee kwa sasa ni kuruhusu njia mpya za kuingiza misaada ya kwenda kutatua changamoto zinazowakabili wananchi walioko Gaza. 

Sauti
3'34"
ICJ-CIJ/ Frank van Beek

Israel yaiambia mahakama ya ICJ kwamba vita dhidi ya Hamas huko Gaza ni kitendo cha kujilinda

Israel imekanusha vikali shutuma kuwa ina nia ya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina na kusisitiza kuwa ipo katika vita ambayo wao hawakuianzisha na wala hawakuitaka kufuatia hapo jana nchi ya Afrika kusini kuwasilisha kesi mbele ya mahakama ya Umoja wa Mataifa ya kimataifa ya haki ICJ wakitaka kukomesha mauaji ya raia huko Gaza.

Sauti
3'4"
UNICEF

Wanawake Rwanda: Tunapaswa tufanye kunyonyesha mahali pa kazi kufanye kazi!

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF Rwanda kwa kushirikiana na wadau kama Shirika la Taifa la Maendeleo ya Mtoto nchini humo, NCDA, wanatoa wito kwa sekta binafsi, taasisi za serikali, washirika, asasi za kiraia kuweka mazingira rafiki ya unyonyeshaji mahali pa kazi. 

Katika moja ya maeneo tulivu ya jiji lenye shughuli nyingi za jiji la Kigali-Rwanda kumetengwa chumba eneo maalumu lenye mazingira yote yanayofaa kwa akina mama kuwanyonyesha Watoto wao au hata kukamua maziwa na kuyahifadhi. 

Sauti
2'34"