Mkataba wa kimataifa juu ya haki za wafanyakazi za majumbani kuanza kufanya kazi mwakani:UM
Mkataba wa Umoja wa Mataifa ambao unaangazia ustawi bora kwa wafanyakazi wa majumbani unatazamiwa kuanza kufanya kazi unaendelea kupata uungwaji mkono baada ya kuridhiwa na mmoja ya nchi wanachama.
Mkataba huo pindi utapoanza kufanya kazi rasmi unatazamia kuinua ustawi wa wafanyakazi wa majumbani zaidi ya milioni moja ambao kwa miaka mingi ustawi wao bado haujazingatiwa.