Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Mkataba wa kimataifa juu ya haki za wafanyakazi za majumbani kuanza kufanya kazi mwakani:UM

Mkataba wa Umoja wa Mataifa ambao unaangazia ustawi bora kwa wafanyakazi wa majumbani unatazamiwa kuanza kufanya kazi unaendelea kupata uungwaji mkono baada ya kuridhiwa na mmoja ya nchi wanachama.

Mkataba huo pindi utapoanza kufanya kazi rasmi unatazamia kuinua ustawi wa wafanyakazi wa majumbani zaidi ya milioni moja ambao kwa miaka mingi ustawi wao bado haujazingatiwa.

Umoja, Mshikamano wa Pamoja ndiyo Njia Bora ya Kutanzua mzozo wa Guinea-Bissau

Mwanadiplomasia wa Umoja wa Mataifa amependekeza hatua zinazopaswa kupitiwa ili kutafutia majawabu mzozo wa kisiasa uliolikumba taifa la Guinea-Bissau lililopo katika pembe ya Afrika Magharibi ambalo hivi karibuni lilishuhudia mapinduzi ya kijeshi.

Taifa hilo hata hivyo linahistoria ya kukumbwa na matukio ya wanajeshi kupoka madaraka tangu lilipojipatia uhuru wake mwaka 1974 toka wa Ureno.