Kashfa za ukatili wa kingono zinapungua- Lacroix
Mwaka 2017 ulikuwa wa majonzi makubwa kwenye operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa.
Mwaka 2017 ulikuwa wa majonzi makubwa kwenye operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa.
Wanamgambo wa kabila la watwa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wamesalimisha mishale 3,000.
Mishale hiyo ilikuwa inatumika kwenye mapigano ya kikabila kati yao ya na jamii wa kabila la wabantu kwenye eneo la Manono lililopo jimbo la Tanganyika.
Msimamizi wa eneo la Manono Pierre Mukamba amesema hatua hiyo ya kusalimisha silaha hizo za kijadi inafuatia mashauriano kati ya ofisi yake na kabila hilo la watwa na tayari silaha hizo zimeteketezwa.
Katika ajenda ya maendeleo endelevu SDGs ya mwaka 2030, lengo namba 3 la afya bora kwa kila mtu, limekuwa changamoto kubwa sana hasa kwa nchi za Afrika zilizoko kusini mwa jangwa la sahara.
Duru ya pili ya uchaguzi nchini Liberia imefanyika hapo jana.
Kufuatia kufanyika kwa duru ya pili ya uchaguzi wa Rais nchini Liberia, Umoja wa mataifa ambao umekuwa ukishirikiana na nchi hiyo katika kuhakikisha amani na utulivu imemmtuma msuluhishi wake kwenda nchini humo.
Msuluhishi huyo ni Rais wa zamani wa Nigeria, Olusegun Obasanjo ambaye amekuwa akifanya jukumu la upatanishi nchini humo.
Bajeti ya umoja wa Mataifa kwa mwaka 2018-2019 yenye kurasa zaidi ya elfu 8 zilizosheheni maelezo ya mipango mbalimbali na takwimu za taasisi hii kubwa zaidi duniani ilipitishwa mwishoni mwa juma na nchi 193 wanachama wa Umoja huo ikiwa na upungufu wa mamilioni ya dola ikilinganishwa na mwaka 2016-2017 unaomalizika. Tuungane na Assumpta Massoi anayetudadavulia zaidi kuhusu kilichomo, kilichoathirika zaidi na matarajio ya baadaye katika kuhakikisha Umoja wa Mataifa unafanya kazi kwa ufanisi na unawajibika kwa nchi wanachama na walipa kodi.
Harakati za kuhamisha kutoka Libya wakimbizi walio hatarini zaidi zinaendelea chini ya usimamizi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR.
Katika hatua ya hivi karibuni zaidi wakimbizi 162 walisafirishwa kwenye Roma, Italia kwa kutumia ndege mbili.
Miongoni mwao ni wanawake, watu wenye ulemavu na watoto waliokuwa wanashikiliwa mateka wakiwa na hali mbaya zaidi.
UNHCR imesema wanawake watano kati yao wakati wanashikiliwa mateka walijifungua watoto bila usaidizi wa kutosha wa matibabu.
Esther, mwenye umri wa miaka 25 aliishi kwa amani na furaha na familia yake huko Kasai, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, lakini ghafla akajikutaka akilazimika kuacha kila kitu chake na kukimbilia yeye na familia yake nchini Angola. Kulikoni? Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
(Taarifa ya Assumpta Massoi)
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amekaribisha hatua iliyofikiwa huko Jamhuri ya Congo baada ya serikali na Frédéric Bintsamou ambaye hujulikana zaidi kama mchungaji Ntumi kutia saini makubaliano ya kusitisha chuki kati yao.
Makubaliano hayo yalitiwa saini mwishoni mwa wiki ambapo Bwana Guterres amesema ni matumaini yake kuwa yatawezesha suluhu ya kudumu na ya amani kwenye mzozo unaoendelea kwenye eneo la Pool.
Nchini Papua New Guinea, wanawake wamechukua hatua kulinda afya zao. Baada ya safari za kutwa kucha kufuata vituo vya afya vilivyokuwa vinapatikana umbali mrefu, wanawake walishikamana na kusaka usaidizi kutoka Benki ya Dunia ili kuanzisha kituo cha afya kwenye kijiji chao. Hatua hii inaenda sambamba na lengo namba 3 la malengo ya maendeleo endelevu, SDG linalotaka nchi wanachama kuhakikisha kuwa kila mtu ana afya nje na ustawi wake unalindwa. Sasa huko Papua New Guinea, hali ilikuwa mbaya hadi wajawazito wanajifungulia watoto kwenye lori.
Mkuu wa operesheni za amani mashinani kwenye Umoja wa Mataifa Atul Khare amesema mradi wa pande tatu unaohusisha Japan, Afrika na Umoja wa Mataifa umezaa matunda katika kuimarisha operesheni za ulinzi wa amani.
Akihojiwa na Idhaa ya Umoja wa Mataifa, Bwana Khare amesema mradi huo unafadhiliwa na Japan na kusimamiwa na Umoja wa Mataifa huku nchi za afrika zikitoa wanajeshi wanaofanyiwa mafunzo ya uhandisi wa kutengeneza vifaa vinavyotumika vitani wakati wa kulinda amani.
(Sauti ya Atul Khare)