Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

© WHO/ Blink Media/Neil Nuia

WHO/UNHCR: Asilimia 75 ya vifo vyote duniani vinatokana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza

Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la afya duniani WHO  na la kuhudumia wakimbizi duniani UNHCR leo yameonya kwamba athari zinazoletwa na magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama vile saratani, magonjywa na mfumo wa hewa na kisukari kwa maisha ya watu duniani ni kubwa huku yakiwa ni chanzo cha asilimia 75 ya vifo vyote. 

Sauti
2'40"
UNICEF Rwanda

UNICEF Rwanda: Programu ya “Winsiga Ndumva” waleta zawadi ya sauti kwa watoto viziwi

Kupitia mradi wa "Winsiga Ndumva", maneno ya lugha ya Kinyarwanda yanayomaanisha "Usiniache nyuma, ninaweza kusikia”, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na wadau wake ikiwemo Wizara ya Afya nchini Rwanda limebadilisha maisha ya watoto wengi na vijana ambao walikuwa na changamoto ya masikio na kuongea kwakuwapatia vifaa maalumu vya kupachika masikioni ili kusaidia masikio kufanya kazi yake ipasavyo. 

Sauti
1'40"
© UNICEF/Karel Prinsloo

Ahunna Eziakonwa: Nimekuja kuona UNDP inavyoweza kuunga mkono maendeleo ya Burundi

Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP Kanda ya Afrika, Ahunna Eziakonwa yuko ziarani nchini Burundi ambako amekutana na makundi mbalimbali ya kijamii na hata kufika mpaka wa Burundi na DRC kuona uhusiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo. Pia Bi. Eziakonwa amekutana na Rais Evariste Ndaishimye.

Sauti
1'47"
© WFP/Michael Castofas

Hali DRC si hali tena, mashirika ya UN yataka msaada zaidi na ulinzi kwa raia

Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la kuhudumia watoto UNICEF na la mpango wa chakula duniani WFP leo yametoa wito wa kuchukuliwa hatua mara moja kuwalinda watoto na familia zao waliojikuta katikati ya machafuko yanayoendelea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, huku lile la kuhudumia wakimbizi UNHCR likielezea wasiwasi mkubwa kuhusu mustakbali wa zaidi ya raia milioni 7 waliotawanywa na kuomba msaada zaidi kutoka jumuiya ya kimataifa.

Sauti
2'31"
©UNMAS/The HALO Trust

Paul Heslop: Uondoaji wa mabomu ya kutengwa ardhini Ukraine ni mtihani na hatari kubwa

Umoja wa Mataifa umesema Ukraine sasa ni moja ya nchi zilizoathiriwa zaidi na mabomu ya kutegwa ardhini duniani huku ikadiriwa kwamba karibu thuluthi moja ya nchi hiyo imeghubikwa na vita eneo ambalo ukubwa wake ni mara nne na nusu ya nchi ya Uswisi. Umoja wa Mataifa umekuwa ukifanya kazi na serikali ya Ukraine kwa miaka 30 na umekuwa ukiongoza mpango wa utekelezaji wa uteguaji wa mabomu ya kutegwa ardhini tangu 2016. 

Sauti
2'33"
© UNHCR/Blaise Sanyila

Bintou Keita: Nina wasiwasi mkubwa na ukikukwaji wa haki za binadamu katika maeneo yanayokaliwa na M23

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Bintou Keita, ameliambia Baraza la Usalama kwamba ana wasiwasi mkubwa kutokana na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na sheria za kimataifa unaofanywa katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa M23, ambapo vuguvugu hilo linalenga watendaji wa mashirika ya kiraia, hasa watetezi wa haki za binadamu na waandishi wa habari. 

Sauti
2'10"
MSC/Marc Muelle

Guterres: Tunahitaji utaratibu wa kimataifa ambao unafanya kazi kwa kila mtu

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo katika mkutano wa usalama unaofanyika mjini Munich Ujerumani ametoa wito wa kuwepo utaratibu wa kimataifa ambao unafanya kazi kwa kila mtu. 

Asante Evarist Guterres katika hotuba yake amesisitiza wito huo wa amani na utaratibu wa kisasa wa kimataifa akisema utaratibu wa leo wa kimataifa haufanyi kazi kwa kila mtu, "Kwa kweli, ningeenda mbali zaidi na kusema kwamba haufanyi kazi kwa mtu yeyote." 

Sauti
2'40"
© UNICEF/Mark Naftalin

Afghanistan: Watoto 683,000 wanufaika na madarasa ya elimu ya kijamii

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto UNICEF linafanya kila juhudi kuhakikisha watoto wanapata mahitaji yao ikiwemo elimu. Huko nchini Afghanistan shirika hilo limehakikisha zaidi ya wanafunzi 683,000 wanapata elimu wangali katika mazingira wanayoishi. 

Mtoto Khadija ni mmoja wa wanufaika wa madarasa ya elimu ya kijamii huko nchini Afghanistan. Kabla ya kuanza kwa programu hii inayofadhiliwa na UNICEF mtoto huyu na wenzake walikuwa hawaendi shule.

Sauti
1'43"