El Niño na janga la tabianchi vyaibua hofu ya ukame Madagascar
El Niño ambao ni mkondo joto, ni hali ya kawaida inayotokea kwenye baharí ikihusisha joto la hewa baharini na wataalamu wanasema unaweza kuvuruga tena kwa kiasi kikubwa mienendo ya hali ya hewa duniani. Hata hivyo dharura ya tabianchi inayosababishwa na shughuli za binadamu zinaongeza ukali na madhara ya El Niño kwa watu na sayari dunia.
Nchini Madagascar, kisiwa ambacho kiko eneo ambamo kimo baharini linakiweka kwenye hatari ya kukumbwa na hali mbaya hewa kupindukia, Umoja wa Mataifa unashirikiana na mamlaka kusaidia taifa hilo kuhimili na kukabili.