Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UN News

Asante Katibu Mkuu kwa kuendelea kuniamini: Elizabeth Mrema

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres Jumanne wiki hii alimtangaza Elizabeth Maruma Mrema kutoka nchini Tanzania kuwa naibu mkurugenzi mtendaji mpya wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira UNEP. 

Bi Mrema tangu mwaka 2020 amehudumu kama katibu mtendaji wa sekretarieti ya mkataba wa Umoja wa Mataifa wa bayoanuai CBD, yenye makao yake makuu mjini Montreal, Canada akizungumza na Idhaa hii ya Kiswahili baada ya uteuzi huo ameelezea alivyoupokea 

(SAUTI YA ELIZABETH MREMA) 

Sauti
2'37"
UN Photo/Eskinder Debebe

Wanafamilia wasema Pelé alikuwa mwenye roho nzuri anayependa Watoto

Ulimwengu umeendelea kuomboleza kwa masikitiko kifo cha mcheza soka wa Brazil Edson Arantes do Nascimento, almaarufu Pelé. Kwa Umoja wa Mataifa Pelé alikuwa mshambuliaji muhimu katika kufanikisha ushindi wa malengo ya Umoja wa Mataifa. Kwa nyakati tofauti akiteuliwa kuwa Balozi Mwema wa mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa kama elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO na kuhudumia watoto UNICEF. UN News kupitia Idhaa ya Kireno imepata fursa ya kuzungumza na mtoto wake wa kiume na mkewe kuhusu Pelé nje ya uwanja.....

Sauti
1'56"
UN Photo/Eskinder Debebe

Jean-Pierre Lacroix akamilisha ziara yake nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR

Mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa Jean-Pierre Lacroix amekamilisha ziara yake nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR ambapo alikutana na walinda amani na kufanya mikutano na viongozi wa kijeshi. Taarifa iliyoandaliwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani CAR, MINUSCA..

Upsound

Nisalamu za kijeshi…… pamoja na gwaride maalum…… ikiwa ni kumkaribisha Mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa Jean-Pierre Lacroix nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR.

Audio Duration
1'50"
© WFP/Gabrielle Menezes

UNCTAD limesema mwaka 2022 umekuwa mgumu ukiziacha familia nyingi zikihaha kuweka mlo mezani

Kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD imesema mwaka huu wa 2022 umekuwa mgumu sana ambapo familia nyingi zimekuwa zikihaha kuweka mlo mezani na kujikimu hadi mwisho wa mwezi, lakini kuna suluhu na suluhu hizo zinapaswa kuwa za kimkakati na za kimataifa.

Kauli hiyo ni kwa mujibu wa Rebeca Grynspan katibu mkuu wa UNCTAD akihojiwa katika kipindi maalum cha UNCTAD Tradecast kuhusu kumalizika mwaka huu wa 2022 na kinachotarajiwa mwakani. 

Sauti
2'7"
Picha: Umoja wa Mataifa/Isaac Billy

Hali si shwari Upper Nile, watoto wakimbia bila mwongozo

Nchini Sudan Kusini mapigano ya kikabila kwenye jimbo la Upper Nile nchini humo yamesababisha vifo, ukimbizi wa ndani halikadhalika madhila zaidi kwa watoto ambao mustakabali wao unazidi kuwa mashakani huku nao wazee wakishuhudia machungu katika taifa hilo changa zaidi duniani.

Nats.. 

Hospitalini Kodok jimboni Upper Nile nchini Sudan Kusini!  

Taswira kutoka video ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa ya kulinda amani nchini humo, UNMISS, ni watoto walio na majeraha! Ya miguu, mgongoni! Wamekata tamaa!! 

Sauti
2'21"
Natanael Melchor/Unsplash

Mwaka 2022 umegubikwa na changamoto lukuki za kiafya na kuweka rehani afya za mamilioni ya watu duniani: WHO

Shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO limesema mwaka 2022 umegubikwa na changamoto lukuki za kiafya , kuanzia janga la COVID-19, Ebola, Mpoxy hadi vita vilivyokatili na kujeruhi wengi hata hivypo linasema kuna matumaini kwa mwaka ujao, yapi?

Taarifa ya tathmini ya kiafya ulimwenguni iliyotolewa leo na WHO nchini Geneva Uswisi imeeleza mwaka 2022, umeendelea kushuhudia uwepo wa janga la COVID-19 pamoja na mlipuko wa ugonjwa wa Mpox hapo awali ikifahamika kama Monkeypox ambao ulienea kwa kasi katika nchi mbalimbali duniani.

Sauti
2'24"
Picha: UNAMA/F. Waezi

UN yataka watalibani wafute uamuzi wao wa kuzuia wasichana kujiunga na Vyuo Vikuu

Umoja wa Mataifa umetaka mamlaka za watalibani nchini Afghanistani kubadili uamuzi wake wa kuzuia wasichana kujiunga na elimu ya Vyuo Vikuu nchini humo ambapo Katibu Mkuu wa Antonio Guterres amesema fursa ya elimu iwe kwa wote huku Mkuu wa haki za binadamu akisema hatua hiyo ni ukiukwaji mkubwa wa wajibu wa AFghanistan katika sheria za kimataifa za haki za binadamu.

Sauti
2'2"
Picha: CBD

UNDP yapongeza COP15 kwa kupitisha makubaliano mapya ya bayonuai kwa ajili ya kulinda mazingira asilia

Ikiwa leo ni tamati ya mkutano wa 15 wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa kuhusu bayonuai, COP15, huko Montréal, Canada, shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo duniani, UNDP, limekaribisha makubaliano ya kihistoria yaliyofikiwa katika mkutano huo kuhusu mpango mpya wa kuhifadhi na kulinda asili kwa kutumia Mfumo mpya wa Kimataifa wa Bayonuai, (GBF) ukipatiwa jina Kunming-Montreal

Sauti
1'54"
Picha: UNFPA/Warren Bright

Dawati la jinsia wilayani Simanjiro nchini Tanzania

Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani na masuala ya afya ya uzazi UNFPA nchini Tanzania limekabidhi jeshi la polisi mkoani Manyara msaada wa jengo la dawati la jinsia na watoto ikiwa njia moja wapo ya jitihada za kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia na mila kandamizi dhidi ya wanawake, wasichana na watoto.

Sauti
4'59"