Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hapa na pale

KM amewasishi wajumbe waliohudhuria Mkutano wa "Mwito wa Cotonou" uliofanyika Ijumatatu, tarehe 12 Oktoba kwenye mji wa Cotonou, Benin, kuzingatia hatari ya biashara ya magendo ya dawa za bandia, kuuhifadhi umma wao na "madhara ya siri na uharamu" wa biashara hiyo. Risala ya KM ilisomwa na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la UM juu ya Maendeleo ya Uchumi kwa Afrika (ECA), Abdoulie Janneh, na iliyahimiza Mataifa Wanachama "kuunganisha uwezo wao kipamoja kupiga vita jinai ya dunia ya kuuza dawa bandia kwa minajili ya masilahi ya afya ya jamii ya kimataifa." Mradi huu wa kampeni ya kuamsha hisia za kimataifa dhidi ya biashara haramu ya dawa za bandia ni uvumbuzi uliobuniwa na raisi mstaafu wa Ufaransa, Jacques Chirac.

Hapa na pale

Ijumamosi ya tarehe 10 Oktoba (2009) huadhimishwa na UM kuwa ni Siku ya Kuwakumbuka Wagonjwa wa Akili Duniani. Risala ya KM kuihishimu siku hii ilieleza siku hii huupatia umma wa kimataifa fursa ya kuhamasisha walimwengu kuchangisha fedha na misaada mengine muhimu inayohitajika kukamilisha malengo ya kutoa uangalizi bora na uuguzaji unaoridhisha wa maradhi ya akili kwa wagonjwa husika, hasa katika mataifa yanayoendelea ambapo mahitaji ya huduma hiyo ni makubwa na uwezo uliopo kukabili janga hilo ni haba sana.

Hali Usomali inasailiwa tena na Baraza la Usalama

Baraza la Usalama asubuhi lilijadilia suala la Usomali kwenye kikao cha hadhara. NKM juu ya Masauala ya Kisiasa, B. Lynn Pascoe na Craig Boyd, ofisa wa Kitengo cha UM Kusaidia vikosi vya Ulinzi Amani vya UA katika Usomali (AMISOM) waliwakilisha ripoti zao kuhusu maendeleo nchini humo.