Hapa na pale
KM amewasishi wajumbe waliohudhuria Mkutano wa "Mwito wa Cotonou" uliofanyika Ijumatatu, tarehe 12 Oktoba kwenye mji wa Cotonou, Benin, kuzingatia hatari ya biashara ya magendo ya dawa za bandia, kuuhifadhi umma wao na "madhara ya siri na uharamu" wa biashara hiyo. Risala ya KM ilisomwa na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la UM juu ya Maendeleo ya Uchumi kwa Afrika (ECA), Abdoulie Janneh, na iliyahimiza Mataifa Wanachama "kuunganisha uwezo wao kipamoja kupiga vita jinai ya dunia ya kuuza dawa bandia kwa minajili ya masilahi ya afya ya jamii ya kimataifa." Mradi huu wa kampeni ya kuamsha hisia za kimataifa dhidi ya biashara haramu ya dawa za bandia ni uvumbuzi uliobuniwa na raisi mstaafu wa Ufaransa, Jacques Chirac.