Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hapa na pale

KM amemteua Dktr. David Nabarro kuwa Mjumbe M aalumu juu ya Udhibitaji Bora wa Lishe na Chakula duniani. Jukumu la Dktr. Nabarro hasa litakuwa ni kumsaidia KM kuhimiza mataifa kutumia miradi ya kizalendo ya kujitegemea chakula maridhawa na udhibiti bora wa lishe, kwa kufuata taratibu za jumla, zenye malengo yalioratibiwa kujumuisha kipamoja mchango muhimu wa mashirika ya kimataifa, ili kukuza misaada inayohitajika kutekelza huduma hizo kwa mafanikio. Tangu mwezi Januari mwaka huu, Dktr. Nabarro alidhaminiwa madaraka ya kushughulikia masuala yanayohusu chakula, na kuandaa taratibu za kuimarisha akiba ya chakula duniani kwa madhumuni ya kutosheleza mahitaji ya umma wa kimataifa.

Hapa na pale

Mfanyakazi mmoja wa Kituo cha Kufyeka Mabomu Yaliotegwa Cyprus (MACC), raia wa Msumbiji, aliuawa leo kwenye ajali iliotukia wakati akiendeleza operesheni zake. Kifo hiki ni cha kwanza kutukia. katika miaka mitano ya shughuli hizi kisiwani Cyprus. Mwaathirika wa ajali hiyo anaitwa Femisberto Novele, na alifariki baada ya bomu liliotegwa kuripuka, katika milango ya saa mbili za asubuhi, kwenye uwanja ulioambukizwa vijibomu viliotegwa ardhini, karibu na sehemu ya Geri, iliopi kilomita 10 kusini-mashariki ya mji wa Nicosia. Taye-Brook Zerihoun, Mjumbe Maalumu wa UM kwa Cyprus na mkuu wa Vikosi vya UM Kulinda Amani Cyprus (UNFICYP) alisema alishtushwa na kuhuzunishwa na ajali iliosababisha kifo cha Novele, tukio ambalo, alitilia mkazo, lilikuwa ni msiba kwa UM, unaokumbusha hatari wanayokabiliwa nayo wafanyakazi wa kimataifa wanaohudumi ufyekaji wa mabomu yaliotegwa, ambayo yamenea katika sehemu kadha katika Cyprus. Zerihoun aliwatumia mkono wa pole ukoo wa marehemu Novele, kwa niaba ya timu ya watumishi wa UM waliopo Cyprus. Mradi wa MACC husimamiwa na Shirika la UM juu ya Miradi ya Maendeleo (UNDP) na tangu 2004, wafanyakazi wa Kituo cha MACC walifanikiwa kuondosha na kuangamiza mabomu 14,000 yaliotegwa, na kusafisha maeneo 57 yaliotegwa mabomu, yanayojumuisha kilomita za mraba milioni 6.5 za ardhi.

Hapa na pale

Baraza la Usalama limekutana leo, awali, kwa mashauriano juu ya Lebanon, na kufuatiwa na mapitio kuhusu vikwazo vilioekewa Cote d\'Ivoire na UM. Ripoti ya mwisho ya Tume Maalumu ya Wataalamu juu ya Cote d\'Ivoire ilithibitisha mzozo wa taifa hili la Afrika Magharibi umeonekana kuchukua sura tofauti, na hauhusu tena mikwaruzano baina ya jimbo la kaskazini na kusini pekee, bali pia inajumlisha makabiliano baina ya wahusika kadha wengineo ambao baadhi yao hupinga rai ya Cote d\'Ivoire kuungana, na wengine wangelipendelea kuona taifa lao linaungana. Ripoti ya Tume ilieleza vile vile eneo la kaskazini linashabihiana, sasa hivi, na mazingira ya uchumi unaoendeshwa na majemadari wa vita (warlords) badala ya sehemu ya taifa ilio chini ya himaya ya serikali. Makamanda wa vita wa kundi la waliokuwa waasi wa Forces Nouvelles wanaosimamia ‘maeneo huru\' wanaoyadhibiti na kunyonya mali ya asili ya Cote d\'Ivoire, ndio sehemu za nchi zinazowachumia mapato. Tume ya Wataalamu ilisema inashughulishwa na tatizo la uhamishaji wa silaha na baruti, pamoja na risasi, kutoka Burkina Faso wanazopelekewa waasi wa Forces Nouvelles, kadhia ambayo Tume ilibashiria hufungamana na biashara ya magendo ya kuuza kakao. Vile vile biashara haramu ya kuuza almasi ilikutikana kufanyika kati ya Cote d\'Ivoire na Burkina Faso na Mali, kwa kupitia Guinea na Liberia, kwa sababu ya ukosefu wa udhibiti wa mipaka baina ya mataifa haya.

UM yajitahidi kuhamasisha Mataifa Wanachama, yatakapokutana Copenhagen, kukamilisha mapatano juu ya udhibiti wa mabadiliko ya hali ya hewa

Janos Pastzor, Mkuu wa Timu ya Ushauri kwa KM juu ya Masuala Yanayohusu Udhibiti wa Athari za Mabadiliko ya Hali ya Hewa alinakiliwa akiwaarifu waandishi habari waliokusanyika kwenye mahojiano yaliofanyika Ijumatatu alasiri katika Makao Makuu, kwamba UM una matarajio ya wastani kuhusu uwezekano wa kuwa na mapatano ya sheria ya kulazimisha, kutokana na mkutano mkuu ujao utakaofanyika mwezi Disemba, katika Copenhagen,