Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watu 160,000 katika JKK watafaidika na msaada wa chakula wa WFP uliovuka kilomita 1,000

Watu 160,000 katika JKK watafaidika na msaada wa chakula wa WFP uliovuka kilomita 1,000

Msafara wa malori 13 yaliobeba chakula, yanayomilikiwa na Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) yamewasili kwenye mji wa Dungu wiki hii, eneo la kaskazini-mashariki katika JKK, baada ya safari ya kilomita 1,000 ambayo ilianzia Uganda, na kupitia Sudan Kusini, hadi Kongo.