Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu ayapongeza Mataifa ya Afrika kwa kuidhinisha chombo kipya cha sheria kulinda haki za wahamiaji wa ndani
Navi Pillay, Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu amekaribisha, kwa furaha kuu, maafikiano ya kuwa na mkataba wa kihistoria kuhusu hifadhi ya wahamiaji wa ndani ya nchi katika Afrika, ambao uliidhinishwa leo hii kwenye Mkutano Mkuu Maalumu wa Wakuu wa Mataifa Wanachama wa Umoja wa Afrika unaofanyika Uganda.