Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UNEP yazitaka nchi za G-20 kuzuia uchafuzi wa mazingira

Wakati viongozi wa dunia wanapokusanyika mjini Seoul nchini Korea Kusini kwenye mkutano wa nchi zilizostawi na zile zinazoinukia kiuchumi za G20, mkurugenzi wa shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa UNEP Achin Steiner ametoa wito kwa viongozi hao kutumia ahadi zao za awali katika kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa na pia katika kujikwamua kutoka kwa hali mbaya ya uchumi.