Mshauri Mstaafu wa Misaada ya Dharura kuzuru Afrika kwa mara ya mwisho
Makamu KM juu ya Masuala ya Kiutu na Misaada ya Dharura, Jan Egeland wiki hii ameanza ziara ya mwisho ya siku 10 katika bara la Afrika kabla ya kustaafu mwisho wa mwaka.
Makamu KM juu ya Masuala ya Kiutu na Misaada ya Dharura, Jan Egeland wiki hii ameanza ziara ya mwisho ya siku 10 katika bara la Afrika kabla ya kustaafu mwisho wa mwaka.
Shirika la UM juu ya Miradi ya Maendeleo (UNDP) limewasilisha rasmi Alkhamisi mjini Cape Town, Afrika Kusini Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu kwa 2006 iliyopewa muktadha usemao “Upungufu wa mahitaji uliovuka mipaka: mzozo wa maji ulimwenguni, ufukara na nguvu za mamlaka.”
Wiki hii mamia ya vijana, kutokea Mataifa Wanachama 192 wa UM, walikusanyika kwa muda wa siku tatu katika Makao Makuu ya UM mjini New York na kujadiliana juu ya taratibu za kudhibiti mchango wao kwenye juhudi za kuyatekeleza Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs).
Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) wiki hii limewakilisha rasmi mchezo mpya wa kompyuta, kwa lugha ya Kiswahili, unaopatikana kwenye mtandao, uliokusudiwa kutumiwa na vijana ili kuwasaidia kwenye zile juhudi za kujifunza mfumo unaoridhisha wa maisha ili, hatimaye, wafanikiwe kujikinga na hatari ya maambukizo ya virusi maututi vya UKIMWI. ~~
Baraza la Usalama pamoja na KM wamewapongeza wazalendo wa JKK (DRC)kwa kufanikiwa kuendeleza upigaji kura wa duru ya pili ya uchaguzi wa uraisi nchini mwao, uliofanyika mwisho wa Oktoba, kwa utulivu wa amani.
KM Kofi Annan ametoa taarifa maalumu, kwa kupitia msemaji wake,iliyoshutumu vikali mashambulio ya hivi karibuni ya kundi moja la wanamgambo wa Sudan yaliyofanyika katika makazi ya eneo la Jebel Moon, Darfur ya Magharibi ambapo iliripotiwa makorja ya raia waliuawa, ikijumuisha pia watoto wadogo. Mashambulio haya yaliwalazimisha maelfu ya raia kuhajiri mastakimu kunusurisha maisha.
Wiki hii Baraza la Usalama limepitisha, kwa kauli moja, azimio la kuongeza kwa miezi sita zaidi opereshani za UM za juu ya ulinzi wa amani katika Sahara ya Magharibi zinazoongozwa na Shirika la MINURSO. Operesheni hizi zinatarjiwa kuendelea hadi mwezi Aprili 2007.
Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limeripoti ya kuwa mnamo wiki mbili zilizopita wahamiaji 800 ziada kutokea jimbo la Casamance la Senegal ya kusini wameyahama makazi yao na kukimbilia vijijini katika taifa jirani la Gambia kujiepusha na mapigano yaliofumka nchini mwao kati ya vikosi vya Serekali na waasi wanaotaka kujitenga, tangu mwezi Agosti mwaka huu.
Majuzi UM ulikamilisha semina ya tano iliyozingatia suala la kustahamiliana kitamaduni, ambayo iliandaliwa na Idara ya Habari (DPI) kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Emory katika Marekani.
UM umeanzisha Mfuko wa Fedha za Kudumisha Amani, waqf ambao umekusudiwa kuzisaidia nchi zinazofufuka kutoka mazingira ya uhasama, fujo, vurugu na vita kufadhiliwa fedha na ujuzi wa kukidhia mahitaji yao ya dharura, hususan katika kipindi ambapo hujikuta zimekabwa kihali na mali kutokana na upungufu wa fedha na ukosefu mkubwa wa zana kufufua ujenzi wa taasisi za taifa zilizoharibiwa na mapigano.~