Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Uzalishaji wa nafaka unaboreka Sudan wakati uhaba wa chakula ukiendelea: FAO
Wakati uhaba wa chakula ukiendelea nchini Sudan, uzalishaji wa nafaka umeimarika kwa kiasi kikubwa Kaskazini Mashariki mwa Afrika, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO.
Ukame Turkana Umeathiri elimu, UNICEF yahaha kusadia watoto kusalia shuleni
Ukame unaoendelea Pembe ya Afrika umeathiri shule zaidi ya 100 katika kaunti ya Turkana Kenya na kusababisha watoto wengi kuacha shule. Sasa shirika la umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Kenya kwa ushirikiano na mradi wa Educate a Child wanaisaidia serikali kusajili watoto shuleni na kuhakikisha waliosajiliwa wanasalia shuleni.
"Niliacha shule nikaenda mitaani, Maisha mitaani yalikuwa magumu sana, njaa kila siku na nilikosa mahali pa kula na kulala.”
Mabadiliko ya tabianchi yanaifanya dunia kutokalika aonya Guterres
Ubinadamu unakabiliwa na ukweli mchungu, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuelekea siku ya hali ya hewa duniani, itakayoadhimishwa kesho Ijumaa akionya kwamba uharibifu ambao tayari umesababishwa na mabadiliko ya tabianchi "unaifanya sayari yetu kutokalika”.
Mustakbali bora unawezekana endapo tutachukua hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi sasa: IPCC Ripoti
Ripoti iliyotolewa na Jopo la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya mabadiliko ya tabianchi (IPCC), inaelezea chaguzi nyingi ambazo zinaweza kuchukuliwa sasa, ili kupunguza uzalishaji wa gesi chafu na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi yanayosababishwa na binadamu.
Jamii Somaliland zasaidiwa kupambana na uhaba wa chakula: FAO
Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO linaendesha mradi wa miaka minne wa mnepo wa uhakika wa upatikanaji wa chakula katika maeneo yaliyoathirika na migogoro pamoja na athari za mabadiliko ya tabianchi katika pembe ya Afrika lengo likiwa ni kujenga amani na kutatua changamoto wanazo kabiliana nazo.
Video ya FAO ikimuonesha Asha Mohammed Ali mama wa watoto 8 na mkulima kutoka wilaya ya Wadaamago huko Somaliland akiwa shambani anapalilia mazao yake huku akisimulia namna ukame ulivyowaathiri wakulima na kuharibu kabisa mustakabali wa maisha yao.
Uwekezaji wa kimkakati unahitajika ili kuboresha uhakika wa chakula na maji kwa mamilioni ya Wasomali
Wakati misaada ya kibinadamu imesaidia baadhi ya maeneo ya Somalia kutotumbukia kwenye baa la njaa, wananchi wa vijiji nchini humo bado wanaendelea kukabiliwa na ukosefu wa uhakika wa chakula limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO hii leo baada ya hivi karibuni kutangazwa matokeo ya uchunguzi wa uhakika wa chakula.
Hakuna tena visingizio, Guterres anatoa wito wa mapinduzi kuzisaidia nchi cha LCD
Viongozi wa dunia wamekusanyika mjini Doha, Qatar kwa mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa unaotaka kuharakisha maendeleo endelevu ambapo usaidizi wa kimataifa unahitajika zaidi ili kufungua uwezo kamili wa nchi zenye maendeleo duni zilizo hatarini zaidi duniani na kuzisaidia kuziweka kwenye njia ya kuelekea ustawi.
Dunia inashuhudia mgogoro wa kihistoria wa chakula huku njaa ikibisha hodi katika milango mingi: OCHA
Mratibu wa umoja wa Mataifa wa masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura Martin Griffiths amesema masuala ya kibinadamu duniani yanakabiliwa na mtihani mkubwa ambao haujawahi kushuhudiwa huku mahitaji yakiongezeka kila uchao duniani kote, migogoro ikipandiana na mamilioni ya watu wakihitaji msaada.
Tulinde ardhi oevu ili itusaidie kupambana na mabadiliko ya tabianchi
Leo ni siku ya ardhi oevu. Umoja wa Mataifa unapigia chepuo siku hii kama njia mojawapo ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi.
Mkutano wa ahadi wa kusaidia bonde la ziwa Chad waanza Niger: OCHA
Serikali za Niger, Ujerumani na Norway, pamoja na Umoja wa Mataifa zinashiriki kwa pamoja mkutano wa 3 wa ngazi ya juu kuhusu Kanda ya bonde la ziwa Chad, ambao umeanza leo tarehe 23-24 Januari katika kituo cha mikutano cha kimataifa cha Mahatma Gandhi huko Niamey, Niger.