Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Wafanyakazi wa IOM wanaosimamia kambi wanafanya kazi katika baadhi ya kambi kubwa za watu waliokimbia makazi yao nchini Somalia.
IOM/Claudia Rosel

Mashirika ya UN yanavyohaha kuwasaidia waathirika wa mizozo na ukame Baidoa Somalia

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO inasema idadi ya milipuko ya magonjwa iliyoripotiwa na dharura za kiafya zinazohusiana na tabianchi katika Ukanda wa Pembe ya Afrika zimefikia kiwango cha juu zaidi kuwahi kutokea karne hii, na hivyo kuzidisha janga la kiafya katika eneo ambalo watu milioni 47 tayari wanakabiliwa na njaa kali. 

Sauti
4'27"
WEF/Pascal Bitz

Guterres atoa onyo kuwa hatuwezi kutatua zahma zinazotukabili katika dunia iliyogawanyika bila mshikamano

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema dunia haiwezi kutatua changamoto kubwa inazokabiliwa nazo hivi sasa kuanzia mabadiliko ya tabianchi, vita ya Ukraine, mdororo wa uchumi na athari zinazoendelea za janga la COVID-19 katikia hali ya sasa ya mgawanyiko na kutokuwa na mshikamano hivyo wakati wa kufumbia macho changamoto hizi umepita na wanaochangia wawajibishwe.

Sauti
2'45"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akihutubia kongamano la kiuchumi duniani WEF, mjini Davos, Uswisi.
© World Economic Forum

Hatuwezi kutatua zahma zinazotukabili katika dunia iliyogawanyika bila mshikamano: Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema dunia haiwezi kutatua changamoto kubwa inazokabiliwa nazo hivi sasa kuanzia mabadiliko ya tabianchi, vita ya Ukraine, mdororo wa uchumi na athari zinazoendelea za janga la COVID-19 katikia hali ya sasa ya mgawanyiko na kutokuwa na mshikamano hivyo wakati wa kufumbia macho changamoto hizi umepita na wanaochangia wawajibishwe.  

Sauti
2'45"
© WFP/Gabrielle Menezes

UNCTAD limesema mwaka 2022 umekuwa mgumu ukiziacha familia nyingi zikihaha kuweka mlo mezani

Kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD imesema mwaka huu wa 2022 umekuwa mgumu sana ambapo familia nyingi zimekuwa zikihaha kuweka mlo mezani na kujikimu hadi mwisho wa mwezi, lakini kuna suluhu na suluhu hizo zinapaswa kuwa za kimkakati na za kimataifa.

Kauli hiyo ni kwa mujibu wa Rebeca Grynspan katibu mkuu wa UNCTAD akihojiwa katika kipindi maalum cha UNCTAD Tradecast kuhusu kumalizika mwaka huu wa 2022 na kinachotarajiwa mwakani. 

Sauti
2'7"