Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
COP27: Unachohitaji kufahamu kuhusu mkutano mkubwa wa Mabadiliko ya Tabianchi wa Umoja wa Mataifa la mwaka huu.
Mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa mkataba wa Kimataifa wa tabianchi COP27 mwaka huu unafanyika huko Sharm el-Sheikh,nchini Misri wakati ambapo dunia inashuhudia ongezeko la hali mbaya ya hewa duniani kote, shida ya nishati iliyochochewa na vita vya Ukraine, na takwimu za wanasayansi zinasisitiza kwamba ulimwengu haufanyi vya kutosha kukabiliana na utoaji wa hewa ya kaboni na kulinda mustakabali wa sayari yetu.
Ufadhili zaidi unahitajika kwa ajili ya kujenga mnepo dhidi ya mabadiliko ya tabianchi:UNEP
Nchi lazima zichukue hatua haraka ili kukabiliana na athari za sasa na zijazo za mabadiliko ya tabianchi, kwani juhudi za sasa ni ndogo sana nana zinafanyika polepole mno, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira (UNEP) katika ripoti yake iliyochapishwa leo.
Mabadiliko ya tabianchi yazidisha zahma ya utapiamlo na njaa Sudan Kusini:UNICEF/FAO/WFP
Umoja wa Mataifa umeonya hii leo kuwa njaa na utapiamlo vinaongezeka katika maeneo yote yaliyokumbwa na mafuriko, ukame na mizozo nchini Sudan Kusini huku baadhi ya jamii zikiwa hatarini kukumbwa na njaa iwapo misaada ya kibinadamu haitakuwa endelevu, halikadhalika mikakati ya kukabili madhara ya mabadiliko ya tabianchi haitaimarishwa.
Nusu ya nchi zote duniani hazina mifumuo ya kutoa taarifa za mapema kuhusu majanga
Ripoti mpya kutoka ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kupunguza hatari za majanga UNDRR na Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa Duniani WMO iliyochapishwa hii leo, imeonya kuwa nusu ya nchi zote duniani kuwa hazina mifumo ya kutoa taarifa za mapema kuhusu majanga.
13 OKTOBA 2022
Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Dunia ipo hatarini kuingia katika mwaka mwingine wenye uhaba wa chakula wakati huu ambapo watu wengi tayari wanazidi kuingia katika dimbwi la uhaba wa chakula, limeonya shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani WFP ambalo limetoa wito wa hatua za haraka kuchukuliwa kushughulikia mzizi wa tatizo hili wakati dunia ikielekea kuadhimisha siku ya chakula duniani hapo Oktoba 16.
11 OKTOBA 2022
Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Umoja wa Mataifa umeshtushwa na ongezeko kubwa la wakimbizi wa ndani huko magharibi kwa Jamhuri ya Kidemokrasia Congo DRC baada ya kuibuka kwa mapigano ya wenyewe kwa wenyewe mwezi Julai huko Kwamouth.
Lengo la kihistoria la ndege zisizozalisha hewa ukaa lakubaliwa katika mkutano wa ICAO
Nchi wanachama wa shirika la kimataifa la usafiri wa anga (ICAO) Ijumaa wamepitisha lengo la muda mrefu la kutozalisha kabisa hewa ukaa ifikapo mwaka 2050, kufuatia wiki mbili za za mkutano wa kikao cha kidiplomasia cha 41 cha Baraza kuu la shirika hilo.
Körösi, akunja jamvi la mjadala wa ngazi ya juu wa UNGA77
Magari yaliyotanda kuzunguka makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kuhakikisha usalama wakati wa wiki ya mjadala wa ngazi ya juu wa viongozi kwenye Baraza Kuu UNGA77 sasa yameondoka na barabara iliyofungwa kufunguliwa, polisi wengi na maafisa wa ujasusi ambao walizuia njia za kuelekea kwenye jengo la Umoja wa Mataifa, nao wametrejea kwenye majukumu yao ya kila siku, kilomita za vyuma vilivyokuwa vizuizi kuzunguka eneo hilo la Umoja wa Mataifa New York, vinavyojulikana kama Turtle Bay navyo vimesafirishwa kwa malori hadi kwenye maghala kusubiri hadi mwakani kwani wiki ya mjadala wa ngazi ya juu imemalizika kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa .
Vita ya Ukraine na Urusi: India iko upande wa amani na itasalia huko
India imesema itaendelezeka ahadi zake za ushirikiano wa pande nyingi, wenye ushahidi uliothibitishwa, uamuzi wa kusambaza chanjo kwa mataifa zaidi ya 100 duniani, kutoa misaada ya maafa kwa wale walio katika taabu, kushirikiana na nchi nyingine, kwa kuzingatia ukuaji wenye kujali mazingira, muungano bora wa kidijitali na upatikanaji wa huduma ya afya.
Ubinadamu uko njiapanda, ni wajibu wetu kuchukua hatua kuunusuru: Ethiopia
Naibu waziri mkuu na waziri wa mambo ya nje wa Ethiopia Demeke Mekonnen Hassen amesema dunia inakabiliwa na mitihani mingi hivi sasa na imejikuta ipo njia panda kuanzia suala la mabadiliko ya tabianchi, umasikini uliokithiri, migogoro, ugaidi na mivutano ya kimataifa.