Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Washiriki wa mkutano wa COP28 wakipita katika ukumbi wa Expo City Dubai.
COP28/Walaa Alshaer

UNESCO yaonya, tunapokumbatia teknolojia tuzingatie hatari yake kwa mabadiliko ya tabianchi

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, leo limetoa ripoti yake ya kwanza kuhusu maadili ya uhandisi wa mabadiliko ya tabianchi likisema kwamba utafiti wa ripoti hiyo unatathmini hatari na fursa za teknolojia mpya za ubadilishanaji na urekebishaji wa masuala ya hali ya hewa na kutoa mapendekezo madhubuti ya utafiti na udhibiti wa tarifa zake.

Maafa yanayohusiana na mabadiliko ya tabianchi kama vile mafuriko, kama inavyoonyeshwa nchini Madagaska, yanaweza kusababisha matatizo mbalimbali ya kiafya.
© UNICEF/Tsiory Andriantsoarana

Walete walio hatarini ‘mbele ya mstari’ wa ufadhili wa tabianchi: COP28

Leo huko Dubai, UAE kwenye Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mazingira, COP28, Akaunti ya Hatua Dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi imezinduliwa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu na Masuala ya Dharura (OCHA) ili kutoa njia ya ziada ya kufadhili hatua za kibinadamu kwenye majanga yanayohusiana na tabianchi kama vile mafuriko, ukame, dhoruba na joto kali, na kujenga uwezo wa kustahimili tabianchi. 

Sauti
2'6"