Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
UNESCO yaonya, tunapokumbatia teknolojia tuzingatie hatari yake kwa mabadiliko ya tabianchi
Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, leo limetoa ripoti yake ya kwanza kuhusu maadili ya uhandisi wa mabadiliko ya tabianchi likisema kwamba utafiti wa ripoti hiyo unatathmini hatari na fursa za teknolojia mpya za ubadilishanaji na urekebishaji wa masuala ya hali ya hewa na kutoa mapendekezo madhubuti ya utafiti na udhibiti wa tarifa zake.
Walete walio hatarini ‘mbele ya mstari’ wa ufadhili wa tabianchi: COP28
Leo huko Dubai, UAE kwenye Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mazingira, COP28, Akaunti ya Hatua Dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi imezinduliwa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu na Masuala ya Dharura (OCHA) ili kutoa njia ya ziada ya kufadhili hatua za kibinadamu kwenye majanga yanayohusiana na tabianchi kama vile mafuriko, ukame, dhoruba na joto kali, na kujenga uwezo wa kustahimili tabianchi.