Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Pampu ya sola Benin yawaepusha vijana na uzururaji wakati wa mwambo
Nchini Benin, mradi unaofadhiliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji, UNCDF umewezesha vijana waliokuwa wanazurura wakati wa msimu wa mwambo nchini humo kuweza kuendelea na shughuli za kilimo kutokana na mradi huo kuwapatia pampu za kusukuma maji ya umwagiliaji kwa kutumia nishati ya sola.
WMO: Ulimwenguni kulikuwa na kiwango cha juu cha joto
Ulimwengu ulikuwa na siku chache za joto kiwango cha juu zaidi kwenye rekodi, kulingana na takwimu za awali zilizotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa WMO.
Türk: Kupambana na mabadiliko ya tabianchi kutalinda haki ya chakula
Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Volker Türk ametoa onyo kali kuhusu hatari ya mabadiliko ya tabianchi kwa haki ya watu kupata chakula akisema “Mazingira yetu yanaungua, yanayeyuka, mafuriko na vyanzo vya maji vinakauka na kufa kabisa."
Wananchi wahamasishwa kuyalinda mazingira baada ya mafuriko Kalehe, DRC.
Muungano wa mashirika ya kiraia katika eneo la Kalehe jimboni Kivu Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wako katika harakati za kuhamasisha wananchi kupanda miti na kuchukua hatua nyingine zitakazosaidia kupambana na mabadiliko ya tabianchi baada ya eneo hilo kukumbwa na mafuriko yaliyosababisha vifo na uharibifu mkubwa mapema mwezi Mei Mwaka huu. Mwandishi wetu wa DRC George Musubao amefika huko na kutuandalia makala ifuatayo. Kwako George.
30 JUNI 2023
Hii leo jaridani tunaangazia wanawake na wasichana nchini Sudan na kazi ya walinda amani nchini CAR. Makala tutakupeleka nchini DRC na mashinani nchini Misri, kulikoni?
Kuimarisha huduma za maji safi nakujisafi kutaokoa maisha ya watu mil 1.4 kwa mwaka
Ingawa huduma za maji safi na kujisafi zimeongezeka katika kipindi cha miaka 10 lakini bado maendeleo hayo ni madogo na hayatoshi kupambana na athari zinazoletwa na ukosefu wa huduma hiyo muhimu imesema ripoti iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO na kuchapishwa na jarida la The Lancet.
DRC maisha yamesambaratishwa na ghasia, kufurushwa na njaa katika mgogoro uliosahaulika: WFP
Jumuiya ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo imetoa ombi la dharura kusaidia mamilioni ya watu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ambako ghasia za muda mrefu na watu kuyakimbia makazi yao kunaendelea kuchochea baa la njaa.
Zaidi ya watu milioni 100 wamelazimika kufungasha virago na kuwa wakimbizi:UN
Katika siku ya wakimbizi duniani Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema wakimbizi wanawakilisha roho bora zaidi ya kibinadamu.
Hatua za haraka zahitajika huku idadi ya wanaolazimika kuhama makwao ikifikia milioni 110: UNHCR
Vita nchini Ukraine, pamoja na migogoro mingine na machafuko yanayotokana na mabadiliko ya tabianchi, vinamaanisha watu wengi zaidi kuliko wakati mwingine wowote walifurushwa makwao mwaka jana, na hivyo kuongeza udharura wa kuchukua hatua za haraka za Pamoja kupunguza janga hilo la kimataifa limesema leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.
Bahari ni sehemu ya suluhisho la matatizo lukuki katika jamii - FAO
Wakati dunia ikijiandaa kuadhimisha siku ya habari duniani hapo kesho Juni nane shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limesema ni vyema jamii kuzingatia afya ya baharí kwani umuhimu wake kamwe hauwezi kupuuzwa.
Bahari, ni makazi ya asilimia 80 ya majani ya wanyama, ambayo yanatumika kama chanzo muhimu cha wananchi kujipatia riziki na pia lishe kwa mamilioni ya watu ulimwenguni.