Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UN News/George Musubao

Wananchi wahamasishwa kuyalinda mazingira baada ya mafuriko Kalehe, DRC.

Muungano wa mashirika ya kiraia katika eneo la Kalehe jimboni Kivu Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wako katika harakati za kuhamasisha wananchi kupanda miti na kuchukua hatua nyingine zitakazosaidia kupambana na mabadiliko ya tabianchi baada ya eneo hilo kukumbwa na mafuriko yaliyosababisha vifo na uharibifu mkubwa mapema mwezi Mei Mwaka huu. Mwandishi wetu wa DRC George Musubao amefika huko na kutuandalia makala ifuatayo. Kwako George.

Sauti
4'38"

30 JUNI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia wanawake na wasichana nchini Sudan na kazi ya walinda amani nchini CAR. Makala tutakupeleka nchini DRC na mashinani nchini Misri, kulikoni?

Sauti
13'4"
Watu waliotawanywa na machafuko wakitembea kurejea eneo la Savo mapema asubuhi karibu baada ya kupata hifadhi katika mji wa karibu wa Bule nchini DRC
© UNHCR/Hélène Caux

Hatua za haraka zahitajika huku idadi ya wanaolazimika kuhama makwao ikifikia milioni 110: UNHCR

Vita nchini Ukraine, pamoja na migogoro mingine na machafuko yanayotokana na mabadiliko ya tabianchi, vinamaanisha watu wengi zaidi kuliko wakati mwingine wowote walifurushwa makwao mwaka jana, na hivyo kuongeza udharura wa kuchukua hatua za haraka za Pamoja kupunguza janga hilo la kimataifa limesema leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR. 

UN Women/BrunoDemeocq

Bahari ni sehemu ya suluhisho la matatizo lukuki katika jamii - FAO

Wakati dunia ikijiandaa kuadhimisha siku ya habari duniani hapo kesho Juni nane shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limesema ni vyema jamii kuzingatia afya ya baharí kwani umuhimu wake kamwe hauwezi kupuuzwa.

Bahari, ni makazi ya asilimia 80 ya majani ya wanyama, ambayo yanatumika kama chanzo muhimu cha wananchi kujipatia riziki na pia lishe kwa mamilioni ya watu ulimwenguni.

Sauti
2'47"