Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mashambulizi ya makombora kutoka angani yamesababisha uharibifu mkubwa kwenye mji wa kusini wa Rafah ulioko Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na Israel
© UNICEF/Eyad El Baba

Habari kwa ufupi:

Mkutano wa kimataifa  kuhusu Gaza wafanyika jijini Paris Ufaransa, FAO inakabiliana na changamoto ya El Niño kwa wakulima na WHO kujenga mifumo ya afya yenye mnepo

UNICEF na Equal Access International, wabuni mbinu za kukabiliana na changamoto katika jamii nchini Kenya. Vijana wahamasishwa kupitia programu za redio.
UNICEF

UNICEF na wadau wake wabuni mbinu za kukabiliana na janga la tabianchi na changamoto katika jamii nchini Kenya

Janga la tabianchi limesababisha kupotea kwa upatikanaji wa elimu, huduma muhimu, na ajira kwa vijana nchini Kenya, hata hivyo Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) nchini humo kwa kushirikiana na shirika la Equal Access International wanawawezesha vijana kuchukua hatua dhidi ya mabadiliko tabianchi na kutoa ufahamu kuhusu suluhisho la kukabiliana na tatizo hilo. 

Sauti
3'37"
UNICEF

UNICEF na Equal Access International, wabuni mbinu za kukabiliana na changamoto katika jamii

Janga la tabianchi limesababisha kupotea kwa upatikanaji wa elimu, huduma muhimu, na ajira kwa vijana nchini Kenya. Hata hivyo Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na Equal Access International wamewawezesha vijana kuchukua hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na kutoa ufahamu kuhusu suluhisho la kukabiliana na tatizo hilo. Evarist Mapesa wa idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa anatufafanulia zaidi katika Makala hii.

Sauti
3'37"

11 OKTOBA 2023

Hii leo jaridani tunaangazia machafuko mashariki ya kati, na mradi wa maji Baringo nchini Kenya. Makala tunakuletea uchambuzi wa Ibara ya 10 ya tamko la haki za binadamu na mashinani tunamulika siku ya mtoto wa kike duniani inayoadhimishwa kila mwaka Oktoba 11 kila mwaka ambayo ni leo.  

Sauti
9'57"
Chini ya nusu ya Nchi Zilizoendelea na chini ya theluthi moja pekee ya Nchi Zinazoendelea za Visiwa Vidogo zina mfumo wa maonyo ya mapema.
© UNDRR/Amir Jina

Nchi zilizo katika bonde la mto Nile kunufaika na mradi wa tahadhari za mapema

Maji yakiwa mengi yanaweza kusababisha mafuriko kama yaliyotokea hivi karibuni huko nchini Libya na uwepo wa maji kidogo unaweza kusababisha ukame kama hali ilivyo kwa nchi nyingi za ukanda wa Jangwa la Sahara kwa sasa, na ndio maana wadau wa masuala ya hali ya hewa wametaka suala la maji kuwa kitovu wakati dunia inashughulikia mabadiliko ya tabianchi. 

UN News

Tunaelimisha wanafunzi na vijana kuhusu mabadiliko ya tabianchi - Madina Jubilate Kimaro

Wiki hii hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kumefanyika mkutano wa tathmini ya malengo ya maendeleo endelevu SDGs kuona wapi nchi wanachama, kampuni, watu binafsi wamefikia kusongesha maendeleo hayo yanayofikia ukomo mwka 2030. Vijana nao walikuwa na siku zao mbili za kuelezea wanafanya nini kule waliko na wanataka nini kifanyike kusongesha malengo hayo likiwemo namba 13 la tabianchi. Miongoni mwa vijana walioshiriki ni Madina Jubilate Kimaro, Balozi wa Mazingira wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani, UNICEF nchini Tanzania.

Sauti
6'24"
Viongozi wa mataifa, wafanyabiashara na mashirika ya kiraia walikusanyika mjini New York kwa ajili ya Mkutano wa Kilele wa Matarajio ya Hali ya Hewa ulioandaliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
© UN News/Anton Uspensky

Muungano wa mabadiliko ya tabianchi wadai hatua, huku Guterres akionya Ubinadamu umefungua milango ya kuzimu

"Joto la kupindukia linaleta madhara ya kutisha duniani ", kwa mujibu wa mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa akizungumza leo katika mkutano wa kwanza kabisa wa ngazi ya juu wa matarajio kuhusu mabadiliko ya tabianchi mbele ya mbele ya muungano wa kimataifa wa kuchagiza hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi ulijumuisha wachagizaji, watendaji, wanasiasa, wafanyabiashara, mashirika ya kimataifa na viongozi wa asasi za kiraia waliokusanyika New York kandoni mwa mjadala wa Baraza kuu UNGA78.