Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Jiungeni na EAC tupate nguvu zaidi ya kuweza kuwasaidia
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Peter Mathuki amezisihi nchi nyingi zaidi zilizopo katika ukanda huo kujiunga na jumuiya yao ili waweze kuwa na nguvu zaidi na pale zitakapokumbwa na changamoto waweze kuwasaidia kwa karibu zaidi kama jumuiya.
Tunakumbatia wito wa kupambana na mabadiliko ya tabianchi kwa vitendo - Vijana Bongoyo Tanzania
Wakati macho na masikio ya Dunia yakielekezwa hapa New York Marekani kwenye mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa utakaoanza Jumatatu wiki ijayo kujadili mada mbalimbali ikiwemo hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi , tunaelekea Tanzania ambako katika pitapita zake, Flora Nducha alipokuwa jijini Dar es Salaama alikutana na mmoja wa vijana wajasiriamali kwenye kisiwa cha Bongoyo waliokumbatia wito wa kupambana na jinamizi la mabadiliko ya tabianchi, akamweleza Flora kuwa mbali ya kujipatia kipato kutokana na utalii endelevu ana jukumu kubwa pamoja na baadhi ya vijana wenzie la kulinda
Kutochukua hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kunaweka rehani maisha ya watu: WMO
Ukosefu wa hatua za kutosha kuelekea utimizaji wa malengo ya mabadiliko ya tabianchi unapunguza kasi ya mapambano ya kimataifa dhidi ya umaskini, njaa na magonjwa hatari, kulingana na ripoti iliyotolewa leo na shirika la hali ya hewa la Umoja wa Mataifa WMO.
Takriban watu 3, 000 wamekufa na 10,000 hawajulikani waliko kufuatia mafuriko Libya:WMO/WHO/IOM/IFRC
Mafuriko makubwa yaliyoikumba Libya tarehe 10 September yamesababisha maafa ikiwemo vifo vya takriban watu 3,000 na wengine zaidi ya 10,000 kutojulikana waliko Mashariki mwa nchi hiyo kwa mujibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na shirikisho la kimataifa la chama cha msalaba mwekundu IFRC na mwezi mwekundu.
Dola Bil 360 zinahitajika kwa mwaka ili kufikia usawa wa kijinsia 2030
Takwimu mpya zilizokusanywa na mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa zimeonesha kuwa kuna haja ya uwekezaji wa ziada wa dola bilioni 360 kwa mwaka ili kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake ifikapo 2030.
Ripoti: Zinahitajika $ Bil 360 kwa mwaka ili kufikia usawa wa kijinsia 2030
Takwimu mpya zilizokusanywa na mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa zimeonesha kuwa kuna haja ya uwekezaji wa ziada wa dola bilioni 360 kwa mwaka ili kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake ifikapo 2030.
UN watoa mwongozo kuhusu haki za watoto katika kupambana na tabianchi
Kamati ya Haki za watoto ya Umoja wa Mataifa leo imechapisha mwongozo kuhusu haki za watoto na mazingira ukitoa maelekezo maalumu kuhusu kupambana na mabadiliko ya tabianchIi.
Mradi wa maji unaotumia sola Benin waepusha vijana na uzururaji wakati wa mwambo
Nchini Benin, mradi unaofadhiliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji, UNCDF umewezesha vijana waliokuwa wanazurura wakati wa msimu wa mwambo nchini humo kuweza kuendelea na shughuli za kilimo kutokana na mradi huo kuwapatia pampu za kusukuma maji ya umwagiliaji kwa kutumia nishati ya sola.
Pampu ya sola Benin yawaepusha vijana na uzururaji wakati wa mwambo
Nchini Benin, mradi unaofadhiliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji, UNCDF umewezesha vijana waliokuwa wanazurura wakati wa msimu wa mwambo nchini humo kuweza kuendelea na shughuli za kilimo kutokana na mradi huo kuwapatia pampu za kusukuma maji ya umwagiliaji kwa kutumia nishati ya sola.
WMO: Ulimwenguni kulikuwa na kiwango cha juu cha joto
Ulimwengu ulikuwa na siku chache za joto kiwango cha juu zaidi kwenye rekodi, kulingana na takwimu za awali zilizotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa WMO.