Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mvulana akitembea kwenye vifusi vya nyumba zilizoharibiwa katika mji wa Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza.
© UNICEF/Eyad El Baba

Mwaka 2024 tishio kwa watoto: Ripoti ya UNICEF

Duniani kote mwaka 2024, watoto wanatarajiwa kuona kuongezeka kwa matukio ya ghasia, vita na matatizo ya kiuchumi, linasema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF), katika utafiti uliotolewa siku ya Jumatatu ya Januari 15, 2024.