Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Guterres atoa wito kwa mkakati mpya wa UN kukabili changamoto za karne ya 21
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo amesisitiza haja ya Umoja wa Mataifa kuimarishwa na kurekebishwa ili kufikia na kusaidia watu kote ulimwenguni.
ILO: Joto la kupindukia linaathiri asilimia 70 yawafanyakazi kote duniani
Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la kazi la Umoja wa Mataifa duniani ILO, inasema zaidi ya asilimia 70 ya wafanyakazi wote duniani wanakabiliwa na uwezekano wa hatari za kiafya kutokana na mabadiliko ya tabianchi.
FAO: Zaidi ya dola mil 16 kuwekezwa kwenye misitu nchini Uganda
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limezindua mradi wa thamani ya euro milioni 15 sawa na dola milioni 16.29 unaofadhiliwa na Muungano wa Ulaya EU ili kusaidia sekta ya misitu ya Uganda kuchangia kwa uendelevu zaidi kwa uchumi na mazingira.
Joto na mafuriko huathiri wanawake na wanaume wa vijijini tofauti na kuongeza tofauti ya kipato
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limezitaka nchi kuhakikisha zinashughulikia changamoto za usawa wa kijinsia kwenye kupambana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi kwani takwimu zinaonesha kuwa familia hususan za vijijini zinazoongozwa na wanawake zinaathirika zaidi na mabadiliko ya tabianchi ikilinganishwa na zile zinazoongozwa na wanaume.
Mkuu wa UN aomba msaada zaidi kwa visiwa vidogo vinavyopambana na mabadiliko ya tabianchi
Ufadhili zaidi unahitajika kusaidia nchi zinazoendelea za visiwa vidogo SIDS, vilivyo katika mstari wa mbele wa mabadiliko ya tabianchi, amesema Jumamosi Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akiwa katika visiwa vya Saint Vincent na Grenada.
Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa ni nini na kwa nini ni muhimu?
Umewadia wakati ambapo nchi zote wanachama wa Umoja wa Mataifa zitapata fursa ya kuonesha kwamba vitendo vya mazingira vinaweza kuunganisha ulimwengu. Wakati huu ni Baraza la Umoja wa Mataifa la Mazingira, au Unea, ambalo mkutano wake wa sita utafanyika kati ya Februari 26 na Machi 1, 2024 Nairobi, Kenya.
Mkutano wa Baraza la Mazingira Duniani UNEA6 wangoa nanga Nairobi Kenya
Mkutano wa sita wa Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa UNEA6 leo umefungua pazia katika Ofisi za Umoja wa Mataifa zilizopo jijini Nairobi, nchini Kenya. Mkutano huo utakaodumu kwa siku tano unahudhuriwa na washiriki zaidi ya 6000 ikiwa ni pamoja na viongozi wa Mazingira duniani, asasi za kiraia, wataalamu wa Mazingira, maofisa waserikali za mitaa, wakulima, vyama vinavyowakilisha wafanyakazi, jamii zilizoachwa nyuma pamoja na maofisa wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa.
Tuangalie mtindo mpya wa ufadhili kwa wakulima na wafugaji waathirika wa mizozo - FAO
Takriban watu milioni 258 katika nchi na maeneo 58 ulimwenguni wanakabiliwa na njaa kali inayochochewa na migogoro ya silaha, majanga ya kiuchumi, mabadiliko ya tabianchi, umaskini na ukosefu wa usawa, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO na kutaka wadau kuangalia upya mtindo wa ufadhili.
FAO yasihi wadau kuangalia mtindo mpya wa ufadhili
Takriban watu milioni 258 katika nchi na maeneo 58 ulimwenguni wanakabiliwa na njaa kali inayochochewa na migogoro ya silaha, majanga ya kiuchumi, mabadiliko ya tabianchi, umaskini na ukosefu wa usawa, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO na kutaka wadau kuangalia upya mtindo wa ufadhili.