Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Margerita, Mwanamke mkulima nchini Sudan Kusini, anapanda mbegu za zao la mahindi. (Maktaba)
FAO/Jean Di Marino

Joto na mafuriko huathiri wanawake na wanaume wa vijijini tofauti na kuongeza tofauti ya kipato

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limezitaka nchi kuhakikisha zinashughulikia changamoto za usawa wa kijinsia kwenye kupambana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi kwani takwimu zinaonesha kuwa familia hususan za vijijini zinazoongozwa na wanawake zinaathirika zaidi na mabadiliko ya tabianchi ikilinganishwa na zile zinazoongozwa na wanaume.

Mkutano wa Sita wa Wazi wa Kamati ya Wawakilishi wa Kudumu (OECPR-6) huko Nairobi, Kenya.
UNEP / Eugene Kaiga

Mkutano wa Baraza la Mazingira Duniani UNEA6 wangoa nanga Nairobi Kenya

Mkutano wa sita wa Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa UNEA6 leo umefungua pazia katika Ofisi za Umoja wa Mataifa zilizopo jijini Nairobi, nchini Kenya.  Mkutano huo utakaodumu kwa siku tano unahudhuriwa na washiriki zaidi ya 6000 ikiwa ni pamoja na viongozi wa Mazingira duniani, asasi za kiraia, wataalamu wa Mazingira, maofisa waserikali za mitaa, wakulima, vyama vinavyowakilisha wafanyakazi, jamii zilizoachwa nyuma pamoja na maofisa wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa.

Sauti
2'23"
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa FAO Beth Bechdol akitembelea Kituo cha Usambazaji wa Virutubisho vya Dharura vya Mifugo huko Isiolo, Kenya. (Maktaba)
FAO/Luis Tato

FAO yasihi wadau kuangalia mtindo mpya wa ufadhili

Takriban watu milioni 258 katika nchi na maeneo 58 ulimwenguni wanakabiliwa na njaa kali inayochochewa na migogoro ya silaha, majanga ya kiuchumi, mabadiliko ya tabianchi, umaskini na ukosefu wa usawa, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO na kutaka wadau kuangalia upya mtindo wa ufadhili.

Sauti
2'40"