Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Ruzuku za IFAD zatunusuru na maambukizi ya COVID-19
Mfuko wa kimataifa wa maendeleo ya kilimo -IFAD umewawezesha wanakijiji nchini Ethiopia kujipatia kipato kupitia mradi wa uchimbaji wa mifereji ya kuzuia maji yasiharibu mazingira na kudhibiti mmonyomoko wa udongo uliokuwa ukiathiri kilimo na hivyo kuwakosesha mapato. Mradi huo pia umewawezesha kujinusuru na maambukizi ya corona.
Mbegu asili matumaini mapya kwa wakazi wa Caatinga Brazil.
Mbegu asilia za mazao zimebaki kuwa tumaini kubwa kwa wakulima wa Caatinga nchini Brazil ambao wameshuhudia athari za mabadiliko ya tabia nchi kutokana na ukataji na uchomaji miti pamoja na ufugaji za mifugo mingi.
UN yatoa wito wa ushirikiano wa kimataifa kupambana na mabadiliko ya tabianchi na kufikia SDGs
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akiongea leo katika mkutano muhimu wa ushirikiano wa kimataifa, amesema ikiwa serikali zitaafikiana kwa pamoja malengo ya kumaliza makaa ya mawe, kuongeza ahadi za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na kuwekeza katika malengo ya dunia, kuna fursa ya kuishinda "changamoto kubwa ya maisha yetu".
Kama si UNICEF na mdau wake Foi En Action, nisingefika popote - Jeannette Niyibigira
Kutokana na mabadiliko ya mifumo ya mvua, hali ambayo imekuwa ikileta maafa nchini Burundi na kusababisha mafuriko, maporomoko ya ardhi na kuharibu mazao, Jeannette Niyibigira, pamoja na mumewe na watoto 5, walilazimika kuyahama makazi yao ya Gatumba, na sasa wanaishi katika kambi ya Kiragaramango ambako kama si mkopo mdogo kutoka shirika la Foi En Action (Faith in Action) ambalo ni wadau wa UNICEF, Camp, maisha yangekuwa magumu zaidi.
Nchi zote lazima zijitolee kupunguza uzalishaji hewa chafunzi – Antonio Guterres
Kutokana na hali mbaya zaidi ya hewa na majanga ya asili, viwango vya juu vya joto na viwango vya juu vya hewa chafuzi, ubinadamu uko kandoni mwa kuzimu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa , António Guterres ameonya hii leo katika mkutano wa tabianchi uliofanyika mjini Petersberg, Ujerumani.
Watu milioni 155 wanakabiliwa na njaa na kuhitaji msaada wa duniani:WFP/FAO/EU
Idadi kubwa na inayoongezeka ya watu wanakabiliwa na njaa kali na wanahitaji msaada wa kuokoa maisha, huku idadi kubwa ya watu wenye njaa kali katika nchi zilizokumbwa na madhila 2020 ilifikia kiwango cha juu zaidi katika miaka mitano, iliyopita imesema ripoti ya kila mwaka iliyozinduliwa leo kwa pamoja na muungano wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa, serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi kushughulikia mgogoro wa chakula.
Dunia iko kitanzini katika mabadiliko ya tabianchi yaonya UN
Viongozi wa dunia lazima wachukue hatua sasa na kuiweka sayari kwenye njia inayojali mazingira kwa sababu "tunaelekea kitanzini", ameonya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo katika hotuba yake kwenye mkutano wa mabadiliko ya tabianchi ulioitishwa na Rais wa Marekani Joseph Biden.
Miongo 3 ya vita dhidi ya amabadiliko ya tabianchi, COVID-19 imetuweka njiapanda:UN
Kwa miaka 28, na kwa wasiwasi unaoongezeka, wanasayansi wakitumia takwimu wamekuwa wakionya juu ya mabadiliko ya tabianchi na athari zake.
Miji ni chachu ya vita dhidi ya mabadiliko ya tabianchi: Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa mifano kadhaa ya jinsi miji ambavyo tayari inafanikiwa katika hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi alipozungumza katika mkutano wa Kikundi cha C40 wa kundi la miji mikubwa ya Uongozi dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, kwani katikati ya miji wameathirika zaidi na jangala corona au COVID-29, na viwango vya juu vya vifo na upotevu wa uchumi.
15 APRILI 2021
Katika jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Grace Kaneiya anakuletea
-Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika watia saini makubaliano ya kusongesha mkataba wa biashara huru barani Afrika ulioanza kutekelezwa rasmi mwaka huu wa 2021
-Nchini Burkina Faso adha ya wazazi wanawake kushindwa kufanyakazi kutokana na kukosa walezi wa watoto imepata dawa baada ya Benki ya Dunia na UNICEF kuanzisha mradi wa vituo vya kulelea watoto