Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mnufaika mwingine kutoka West Guji, akishikilia mbuzi aliowanunua akitumia msaada w apesa taslim. Picha: IOM Ethiopia
Picha: IOM Ethiopia

Ruzuku za IFAD zatunusuru na maambukizi ya COVID-19

Mfuko wa kimataifa wa maendeleo ya kilimo -IFAD umewawezesha wanakijiji nchini Ethiopia kujipatia kipato kupitia mradi wa uchimbaji wa mifereji ya kuzuia maji yasiharibu mazingira na kudhibiti mmonyomoko wa udongo uliokuwa ukiathiri kilimo na hivyo kuwakosesha mapato. Mradi huo pia umewawezesha kujinusuru na maambukizi ya corona.

Sauti
2'23"
Mji Mkuu wa Jamhuri ya Kofrea , Seoul
Unsplash/Chinh Le Duc

UN yatoa wito wa ushirikiano wa kimataifa kupambana na mabadiliko ya tabianchi na kufikia SDGs

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akiongea leo katika mkutano muhimu wa ushirikiano wa kimataifa, amesema ikiwa serikali zitaafikiana kwa pamoja malengo ya kumaliza makaa ya mawe, kuongeza ahadi za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na kuwekeza katika malengo ya dunia, kuna fursa ya kuishinda "changamoto kubwa ya maisha yetu".

Jeannette Niyibigira, mshoni na mnufaika wa mkopo unaofadhiliwa na UNICEF na shirika la kiraia la Foi en Action akisalimia wakazi wenzake wa kambi ya wakimbizi wa ndani ya Gatumba karibu na mji wa Bujumbura nchini Burundi.
© UNICEF/Karel Prinsloo

Kama si UNICEF na mdau wake Foi En Action, nisingefika popote - Jeannette Niyibigira 

Kutokana na mabadiliko ya mifumo ya mvua, hali ambayo imekuwa ikileta maafa nchini Burundi na kusababisha mafuriko, maporomoko ya ardhi na kuharibu mazao, Jeannette Niyibigira, pamoja na mumewe na watoto 5, walilazimika kuyahama makazi yao ya Gatumba, na sasa wanaishi katika kambi ya Kiragaramango ambako kama si mkopo mdogo kutoka shirika la Foi En Action (Faith in Action) ambalo ni wadau wa UNICEF, Camp, maisha yangekuwa magumu zaidi.

Mama akiandaa chakula kwa ajili ya binti yake kwa kutumia nafaka alizozipata kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la  mpango wa chakula, WFP, Maiduguri, Nigeria.
© WFP/Oluwaseun Oluwamuyiwa

Watu milioni 155 wanakabiliwa na njaa na kuhitaji msaada wa duniani:WFP/FAO/EU 

Idadi kubwa na inayoongezeka ya watu wanakabiliwa na njaa kali na wanahitaji msaada wa kuokoa maisha, huku idadi kubwa ya watu wenye njaa kali katika nchi zilizokumbwa na madhila 2020 ilifikia kiwango cha juu zaidi katika miaka mitano, iliyopita imesema ripoti ya kila mwaka iliyozinduliwa leo kwa pamoja na muungano wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa, serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi kushughulikia mgogoro wa chakula. 

Miji kama mji mkuu wa Korea Kusini Seoul ni watumiaji wakubwa wa nishati
Unsplash/Ethan Brooke

Miji ni chachu ya vita dhidi ya mabadiliko ya tabianchi: Guterres 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa mifano kadhaa ya jinsi miji ambavyo tayari inafanikiwa katika hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi alipozungumza katika mkutano wa Kikundi cha C40 wa kundi la miji mikubwa ya Uongozi dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, kwani katikati ya miji wameathirika zaidi na jangala corona au COVID-29, na viwango vya juu vya vifo na upotevu wa uchumi.  

15 APRILI 2021

Katika jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Grace Kaneiya anakuletea

-Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika watia saini makubaliano ya kusongesha mkataba wa biashara huru barani Afrika ulioanza kutekelezwa rasmi mwaka huu wa 2021

-Nchini Burkina Faso adha ya wazazi wanawake kushindwa kufanyakazi kutokana na kukosa walezi wa watoto imepata dawa baada ya Benki ya Dunia na UNICEF kuanzisha mradi wa vituo vya kulelea watoto

Sauti
14'41"