Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Tishio la mabadiliko ya tabianchi linaendelea kuongezeka Afrika:WMO Ripoti
Ripoti mpya iliyotolewa na shirika la Umoja wa utabiri wa hali ya hewa WMO ikitanabaisha hali ya sasa na mustakabali wa hali ya hewa katika bara la Afrika inaonyesha kwamba mwaka 2019 ulikuwa miongoni mwa miaka mitatu yenye joto la kupindikia katika historian a mwenendo unatarajiwa kuendelea ukisababisha watu kutawanywa na athari katika kilimo.
26 Oktoba 2020
Ripoti yabaini magari mengi yanayopelekwa nchi za uchumi mdogo hayafai.
Ukosefu wa ajira na makazi salama vyawaacha wafanyakazi wahamiaji hatarini Lebanon, imesema IOM.
Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO huko nchini Madagascar linatekeleza mradi wa kuhakikisha kuwa wakazi wanaoishi karibu na eneo la hifadhi la Makira wanakuwa na uhakika wa kupata mlo bora bila kusambaratisha eneo hilo la hifadhi.
Vijana Kenya wavumbua apu ya simu itakayosaidia katika upandaji miti
Miti huchangia kwa kiwango kikubwa katika kutunza mazingira kwa kuzuia kuenea majangwa kupitia kuleta mvua na pia kutunza vyanzo vya maji ardhini. Kwa upande wa uchumi hali kadhalika, miti ina manufaa kama vile mbao.
Wakati ni sasa kuchukua hatua kukomesha uchafuzi wa hewa:Guterres
Watu 9 kati ya 10 wanavuta hewa chafu, ni wakati wakubadili hilo sasa Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema huu ni wakati wa kushikamana na kuchukua hatua zinazohitajika dhidi ya hewa chafu inayovutwa na watu 9 kati ya 10 kila uchao duniani kote. Assumpta Massoi na taarifa zaidi
(TAARIFA YA ASSUMPTA MASSOI)
Kupitia ujumbe wake wa maadhimisho ya kwanza kabisa ya siku ya kimataifa ya hewa safi kwa ajili ya anga ya blu, Guterres ameonya kwamba hewa chafu inayovutwa inachangia kwa kiasi kikubwa magonjwa ya moyo, kiharusi,
07 SEPTEMBA 2020
Katika Jarida la Habnari la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Katika maadhimisho ya kwanza kabisa ya siku ya kimataifa ya hewa safi kwa ajili ya anga ya rangi ya blu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametaka mshikamano kutokomeza uchafuzi wa hewa
-Nchini Pakistan mbinu za kupambana na ugonjwa wa Polio zawa mkombozi mkubwa katika vita dhidi ya corona au COVID-19 ikiwemo miundombinu yake
-Waalimu, wanafunzi na wazazi nchini Uganda waelezea changamoto za kusomea nyumbani wakati huu wa janga la corona au COVID-19
Watu 9 kati ya 10 wanavuta hewa chafu, ni wakati wa kubadili hilo sasa:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema huu ni wakati wa kushikamana na kuchukua hatua zinazohitajika dhidi ya hewa chafu inayovutwa na watu 9 kati ya 10 kila uchao duniani kote.
Ziwa Turkana hatarini kukauka, uhai wa wanaolitegemea mashakani
Nchini Kenya, ziwa Turkana ambalo ni ziwa kubwa la kudumu lililoko jangwani liko hatarini kukauka na hivyo kutishia uhai wa watu zaidi ya 300,000 wanaotegemea kipato chao kutokana na maji yake.
Hali ya hewa ya Morogoro haikuwa hivi, hatua za pamoja na za haraka zinahitajika-Wakazi wa Morogogo
Mkoa wa Morogogoro ulioko katika eneo la mashariki la Tanzania ni moja ya maeneo ambayo kwa miaka mingi yametambulika kuwa maeneo yenye hali nzuri ya hewa kutokana na mazingira yake kuwa yenye misitu, nyika, na milima yenye kutiririsha maji safi. Lakini katika miaka ya hivi karibuni wanaharakati wa kutunza mazingira wanaona kuwa ni muhimu kuchukua hatua za kuilinda hali hiyo kwani iko katika hatari ya kutoweka kutokana na shughuli za binadamu kama vile uchomaji mkaa.
05 Agosti 2020
-Na le
Moto na kuyeyuka kwa barafu Arctic vyahitaji hatua za haraka dhidi ya mabadiliko ya tabianchi:WMO
Shirika la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO leo limesema joto kali la kupindukia na la muda mrefu Siberia limesababisha sehemu ya Arctic kuwa na joto kuliko kawaida na kuchochea kuzuka kwa moto wa nyika kwa mwaka wa pili mfululizo huku likionya pia kuhusu kupungua kwa kasi kwa barafu baharini kwenye pwani ya Urusi.