Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

22 MACHI 2021

Katika jarida la mada kwa kina hii leo kutoka Umoja wa Mataifa Grace Kaneiya anakuletea

-Leo ni siku ya maji duniani na Umoja wa Mataifa umesisitiza kila mtu kutambua thamani ya rasilimali hiyo muhimu ili kuhakikisha watu wote wana fursa ya kuipata kote duniani

-Nchini Sudan Kusini mpango wa Umoja wa Mastaifa UNMISS umeendesha warsha ya siku mbili Yambio na Nzara kwa ushirikiano na serikali ili kuhakikisha vijana, wanawake na jamii wanajikwamua vyema na janga la COVID-19, vita na mabadiliko ya tabianchi

Sauti
12'33"

18 Februari 2021

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanza na masuala ya mazingira ambapo ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa inasema bado safari ni ndefu kukabili mabadiliko ya tabianchi. Kisha anabisha hodi Msumbiji ambako anaangazia msaada kwa manusura wa dhoruba kali Eloise. Baada ya hapo anakwenda baharí Hindi visiwani Comoro ambako mradi wa shirika la kazi duniani, ILO umeleta ajira za staha kwa wakazi maskini. Makala tunarejea tena Tanzania jijini Dar es salaam kumulika kilimo cha mboga mboga na matumizi ya muarobaini kukabili wadudu waharibifu.

27 Januari 2021

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanzia nchini Tanzania kumulika harakati za watoto wa kike na elimu, kisha anakukutanisha na wajasiriamali vijana kupitia shirika la maendeleo ya viwanda la Umoja wa Mataifa, UNIDO. Baada ya hapo anakupeleka Vietnam ambako utaalamu umemaliza tabia ya wakulima kuonja maji ili kutambua iwapo yana chumvi nyingi au la kabla ya kumwagilia kwenye mpunga. Makala tunakwenda Nairobi nchini Kenya ambako kijana aliyekuwa sugu mtaani sasa amegeuka mkombozi kwa vijana wengine waliokuwa tishio mitaani na anatamatisha na mashinani kutoka Sudan Kusini, karibu!

Sauti
13'43"