Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Bila kuishi kwa amani na mazingira asilia hatma yetu ni mtihani:Guterres
Katubu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema dunia inahitaji kuwa na amani mazingira asili kwani bila msaada wa mazingira asilia hakuna uhai na hakuna maisha katika sayari hii.
Bahari na mustakbali wa dunia viko hatarini kutoka na mabadili ya tabianchi:WMO
Katika kuelekea siku ya utabiri wa hali ya hewa duniani hapo kesho machi 23, shirika la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO, limesema bahari huendesha hali ya hewa duniani na huimarisha uchumi na uhakika wa chakula.
22 MACHI 2021
Katika jarida la mada kwa kina hii leo kutoka Umoja wa Mataifa Grace Kaneiya anakuletea
-Leo ni siku ya maji duniani na Umoja wa Mataifa umesisitiza kila mtu kutambua thamani ya rasilimali hiyo muhimu ili kuhakikisha watu wote wana fursa ya kuipata kote duniani
-Nchini Sudan Kusini mpango wa Umoja wa Mastaifa UNMISS umeendesha warsha ya siku mbili Yambio na Nzara kwa ushirikiano na serikali ili kuhakikisha vijana, wanawake na jamii wanajikwamua vyema na janga la COVID-19, vita na mabadiliko ya tabianchi
Nishati jadidifu ni chachu ya maendeleo na mustakbali wa amani:UNEP
Nishati mbadala au jadidifu ni "muhimu kwa kujenga mustakbali endelevu, ustawi na amani", amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akizindua harakati za kuongeza kasi kwa ajili ya nishati safi na hatua kwa ajili ya kukabili mabadiliko ya tabianchi.
UN yapokea kwa furaha kurejea rasmi kwa Marekani katika Mkataba wa Paris.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, amesema "kiunganishi kilichokosekana kilidhoofisha jambo zima" akiwa anaeleza kipindi ambacho Marekani haikuwepo katika utekelezaji wa mkataba wa Paris unaolenga kupambana na mabadiliko ya tabianchi.
Dunia bado inaweza kutatua changamoto ya mabadiliko ya tibianchi, kutimiza SDGs na kuishi vyema na mazingira:UN
Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP inatoa muongozo wa jinsi ya kushughulikia changamoto kubwa tatu za dharura zinazoikumba dunia ambazo ni mabadiliko ya tabianchi, kuishi vyema na mazingira na ufikiaji wa malengo ya maendeleo endelevu SDGs.
18 Februari 2021
Hii leo jaridani Flora Nducha anaanza na masuala ya mazingira ambapo ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa inasema bado safari ni ndefu kukabili mabadiliko ya tabianchi. Kisha anabisha hodi Msumbiji ambako anaangazia msaada kwa manusura wa dhoruba kali Eloise. Baada ya hapo anakwenda baharí Hindi visiwani Comoro ambako mradi wa shirika la kazi duniani, ILO umeleta ajira za staha kwa wakazi maskini. Makala tunarejea tena Tanzania jijini Dar es salaam kumulika kilimo cha mboga mboga na matumizi ya muarobaini kukabili wadudu waharibifu.
27 Januari 2021
Hii leo jaridani Flora Nducha anaanzia nchini Tanzania kumulika harakati za watoto wa kike na elimu, kisha anakukutanisha na wajasiriamali vijana kupitia shirika la maendeleo ya viwanda la Umoja wa Mataifa, UNIDO. Baada ya hapo anakupeleka Vietnam ambako utaalamu umemaliza tabia ya wakulima kuonja maji ili kutambua iwapo yana chumvi nyingi au la kabla ya kumwagilia kwenye mpunga. Makala tunakwenda Nairobi nchini Kenya ambako kijana aliyekuwa sugu mtaani sasa amegeuka mkombozi kwa vijana wengine waliokuwa tishio mitaani na anatamatisha na mashinani kutoka Sudan Kusini, karibu!
Badala ya kuonja maji kutambua kiwango cha chumvi, sasa wakulima watumia simu ya kiganjani
Nchini Vietnam, mfuko wa maendeleo ya Umoja wa Mataifa, IFAD umesaidia wakulima kuondokana na tabia ya kuonja maji ya umwagiliaji ili kutambua kiwango cha chumvi na badala yake sasa wanatumia teknolojia ya simu ya kiganjani ili kuongeza mavuno ya mpunga
Raia wa Burkina Faso wanazikimbia vurugu, wanapokelewa na madhara ya mabadiliko ya tabianchi
Nchini Burkina Faso, watu waliofurushwa katika makazi yao, wanahangaika kutafuta kimbilio dhidi ya vurugu na athari za mabadiliko ya tabianchi. Baada ya kuacha nyumba zao, ambako ukame umekuwa wa kawaida, maelfu ya watu wakati huo huo wanakabiliwa na mafuriko makali ambayo yalifuta makazi yao.