Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi: Ni wakati wa kutengeneza amani na asili-Katibu Mkuu wa UN
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres, ameelezea mapambano dhidi ya janga la mabadiliko ya tabianchi kama kipaumbele cha juu kwa karne ya 21, kupitia hotuba yake aliyoitoa Jumatano hii katika Chuo Kikuu cha Columbia mjini New York Marekani.
Dunia inahitaji kuchukua hatua zaidi kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi-UNHCR
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, kesho Jumatano likifanya mkutano wa ngazi ya juu kushughulikia athari za mabadiliko ya tabianchi kwa wakimbizi na wakimbizi wa ndani, pamoja na wengine walio katika mazingira hatarishi kote, mshauri maalumu wa UNHCR kuhusu mabadiliko ya tabianchi Andrew Harper amesema dunia inapaswa kuchukua hatua kali zaidi kwani mabadiliko ya tabia nchi huwezi kuyavalia barakoa.
COVID-19, vita na mabadiliko ya tabianchi vyaongeza zahma ya utapiamlo Afghanistan:WFP
Nchi ya Afghanistan inakabiliwa na changamoto kubwa ya kutokuwa na uhakika wa chakula huku viwango vya utapiamlo vikifurutu ada kutokana na tishio litokanalo na majanga matatu makubwa ambayo ni vita, corona au COVID-19 na mabadiliko ya tabianchi kwa mujibu wa shirika la umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP.
Wazee wazungumza historia ya mafuriko kwenye Ziwa Albert
Maelfu ya watu wanendelea kuathiriwa na mafuriko yanayoshuhudiwa katikaa meneo mbalimbali hasa yale ya Ziwani nchini Uganda.
Licha ya onyo kutoka kwa serikali na asasi za kiraia kuwa mafuriko haya yanaweza kuendelea, mpaka sasa baadhi ya watu wanahama mita chache wakiwa na matumaini kwamba maji haya yatapungua mambo yarejee kama kawaida.
Hata hivyo, watu wa asili kwenye Ziwa Albert wanaonya kuwa mambo bado kutokana na mfano kama huo ulioshuhudiwa na waliokuwepo miaka ya elfu moja kendamia sitini.
16 Novemba 2020
Ungnana na Flora Nducha katika habari la leo Jumatatu Novemba 16, 2020
Janga la COVID-19 linajaribu hatua zilizopigwa katika maendeleo
Janga la corona au COVID-19 linabadili hatua zilizopigwa katika maendeleo na kuujaribu msingi wa amani ya kimataifa, lakini pia linatoa fiursa ya kushirikiana kuzisaidia serikali na jamii kujijenga vyema upya umesema mkutano wa kimataifa ulioanza leo kwa njia ya mtandao mjini Roma Italia ukiwaleta pamoja wawakilishi wa Umoja wa Mataifa, taasisi za fedha za kimataifa, Muungano wa Afrika naserikali za Muungano wa Ulaya.
Ushirikiano ndio jawabu pekee la kukabili changamoto za dunia hivi sasa:Guterres
Janga la corona au COVID-19 linabadili hatua zilizopigwa katika maendeleo na kuujaribu msingi wa amani ya kimataifa, lakini pia linatoa fiursa ya kushirikiana kuzisaidia serikali na jamii kujijenga vyema upya umesema mkutano wa kimataifa ulioanza leo kwa njia ya mtandao mjini Roma Italia ukiwaleta pamoja wawakilishi wa Umoja wa Mataifa, taasisi za fedha za kimataifa, Muungano wa Afrika naserikali za Muungano wa Ulaya.
Mabadiliko ya tabianchi yskishuhudiwa Niger, IFAD yatoa muarobaini
Nchini Niger, mfuko wa maendeleo ya kilimo wa Umoja wa Mataifa, IFAD kwa kushirikiana na serikali unasaidia wazalishaji wadogo wa nafaka hususani vikundi vya wanawake katika eneo la Mouradi ambao mabadiliko ya hali ya hewa yameathiri sana maisha yao ili waweze kukabiliana na hali inayobadilika na pia majanga ya baadaye.
IFAD yasaidia wanawake wa Mouradi, Niger kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi
Nchini Niger, mfuko wa maendeleo ya kilimo wa Umoja wa Mataifa, IFAD kwa kushirikiana na serikali unasaidia wazalishaji wadogo wa nafaka hususani vikundi vya wanawake katika eneo la Mouradi ambao mabadiliko ya hali ya hewa yameathiri sana maisha yao ili waweze kukabiliana na hali inayobadilika na pia majanga ya baadaye.
UN yaipongeza Jamhuri ya korea kwa ahadi ya kukomesha uzalishaji wa hewa ukaa
Ahadi ya Jamhuri ya Korea ya kufanikisha kutokuwepo kwa hewa ukaa ifikapo mwaka 2050 imepongezwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kama “Ni hatua nzuri sana katika mwelekeo sahihi”