Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

27 Oktoba 2021

Karibu kusikiliza jarida ambapo leo tunakuletea mada kwa kina maalum kutokea Beni jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC ikimulika michezo hususan mpira wa miguu na ulinzi wa amani ambako kumefanyika  mechi ya kirafiki kati ya Timu ya walinda amani kutoka Tanzania na wenyeji Lion Mavivi.

Pia utapata fursa ya kusikiliza habari kwa kifupi zikiangazia makubaliano ya kusambazwa dawa ya vidonge vya kutibu COVID-19 kwa wagonjwa wasio mahututi, utasikia pia shughuli mbalimbali zinazofanywa na Umoja wa Mataifa mashinani nchini Tanzania.

Sauti
11'38"
© Unsplash

Dunia bado ipo hatarini kuwa na ongezeko la joto : UNEP

Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP imeeleza kuwa ahadi mpya na zilizorekebishwa kuhusu viwango vya nchi vya kukabili mabadiliko ya tabianchi, NDCs hazijafikia lengo lililowekwa katika mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi na hivyo ulimwenguni kuwa hatarini kuwa na ongezeko la joto la angalau nyuzijoto angalau 2.7 katika karne hii
 
(Leah Mushi na taarifa zaidi.)

Sauti
1'17"

26 Oktoba 2021

Karibu usikilize jarida ambapo leo Assumpta Massoi amekuandalia habari mbalimbali zikiwemo

Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP imeeleza kuwa ahadi mpya na zilizorekebishwa kuhusu viwango vya nchi vya kukabili mabadiliko ya tabianchi, NDCs hazijafikia lengo lililowekwa katika mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi na hivyo ulimwenguni kuwa hatarini kuwa na ongezeko la joto la angalau nyuzijoto angalau 2.7 katika karne hii.

Sauti
11'59"
© UNICEF/Helene Sandbu Ryeng

Mafuriko yawatenga wananchi kwa miezi 6 bila msaada wowote nchini Sudan Kusini

Mvua kubwa zilizonyesha katika kipindi cha miezi 6 iliyopita nchini Sudani Kusini zimeathiri miundombinu ya barabara, madaraja na viwanja vya ndege huku zaidi ya wakazi  700,000 wa kaunti ya Maban jimboni Jonglei wakisalia wakiiishi bila kupata msaada wowote kutokana na eneo lote kujaa maji.
Wafanyakazi wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia wakimbizi UNHCR kwa kutumia helipokta wameweza kufika eneo hilo na Leah Mushi anatuletea taarifa kamili.

ADB/Ariel Javellana
Uzalishaji kutoka kwa mitambo ya kufua umeme wa makaa ya mawe unachangia uchafuzi wa hewa huko Ulaanbaatar, Mongolia.

Uzalishaji wa mafuta ya kisukuku unapeleka kombo malengo ya mabadiliko ya tabianchi:UNEP

Licha ya kuongezeka kwa matarajio ya mabadiliko ya tabianchi na ahadi za kutokomeza kabisa uzalishaji wa hewa ukaa, serikali bado zina mpango wa kuzalisha zaidi ya mara mbili ya kiwango cha nishati kutoka kwenye mafuta ya kisukuku ifikapo mwaka 2030, kuliko kiwango ambacho kitapunguza ongezeko la joto duniani hadi kufikia kiwango kilichowekwa kwenye mkataba wa Paris cha nyuzijoto 1.5 katika kipimo cha Selsiasi (1.5° C)

Mabadiliko ya hali ya hewa kwa mfano ukame yanasababisha athari za kiuchumi miongoni mwa wakulima.
UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Afrika inakabiliwa na hatari kubwa ya mabadiliko ya tabianchi:WMO

Ripoti mpya iliyotolewa leo na mashirika mbalimbali na kuratibiwa na shirika la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO imesema mabadiliko ya mifumo ya mvua, kuongezeka kwa joto na hali mbaya ya hewa kumechangia kuongezeka kwa ukosefu wa chakula, umaskini na watu kutawanywa barani Afrika mwaka 2020 huku hali mbaya ikizidishwa nachangamoto za kijamii, kiuchumi na kiafya ziliyosababishwa na janga la COVID-19.