Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Biden airejesha Marekani WHO na mkataba wa Paris; UN yapongeza
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, muda mfupi uliopita mjini New York Marekani, amekaribisha hatua ya Rais mpya wa Marekani Joe Biden kuirejesha Marekani katika Mkataba wa Paris mabadiliko ya tabianchi.
14 Januari 2021
Hii leo jaridani kwa kiasi kikubwa ni masuala ya mabadiliko ya tabianchi tukimulika ripoti ya shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP, kuhusu hatua thabiti za kuhimili mabadiliko ya tabianchi na kutumia mbinu za asili, halikadhalika ripoti kuhusu viwango vya joto kutoka shirika la hali ya hewa la Umoja wa Mataifa, WMO, ikiutaja mwaka 2020 kuwa moja ya miaka mitatu iliyoongoza kwa kuwa na viwango vya juu sana vya joto duniani. Tunakwenda pia huko Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR ambako mapigano mapya yamesababisha vikosi vya walinda amani wa Umoja wa Mataifa kuchukua hatua.
Tujenge mnepo dhidi ya mabadiliko ya tabianchi au tukabiliwe na zahma ya kiuchumi na kibinadamu:UNEP
Karibu robo tatu ya mataifa kote duniani yameweka mipango ya kukabiliana na kuhimili mabadiliko ya tabianchi, lakini ufadhili na utekelezaji unaohitajika wa mipango hiyo ndio mtihani mkubwa kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP.
Mradi wa kuboresha mazingira Sahel GGW wapigwa jeki ya dola zaidi ya bilioni 14
Mradi kabambe wa kukabiliana na hali ya jangwa kwenye ukanda wa sahel na Sahara wa Great Green Wall, GGW umepokea ufadhili wa dola bilioni 14.236 za kimarekani.
05 JANUARI 2021
Katika Jarida la Habari za UN hii leo Flora Nducha anakuletea
-Wakimbizi kutoka Tigray Ethiopia waendelea kumiminika Sudan na mahitaji yao yanaongezeka lasema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR
-Kutana na Muhamiaji Mohammed Bushara ameye alienda Libya kusaka mustakbali bora lakini sasa amerejea nyumbani kwa msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM na Muungano wa Ulaya Eu na kuanzisha biashara ya duka la vipodozi
Kijana Nkosi wa Zimbabwe atumia kipaji chake cha kuongea, kutetea tabianchi
Nchini Zimbabwe kijana mdogo wa umri wa miaka 17 anatumia kipaji chake cha kuongea kuhamasisha mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.
21 DESEMBA 2020
Hii leo jaridani ni mada kwa kina na tunakwenda mkoani Mwanza nchini Tanzania ambako shirika la Amani girls home wameanzisha mradi unaowawezesha wasichana hususani wale waliokumbwa na changamoto mbalimbali za kimaisha, ili waweze kufikia malengo yao kwa kuwapa ujuzi mbalimbali. Lakini tuna Habari kwa Ufupi ikimulika Burkina Faso, Mali na kubabuka kwa matumbawe Mashinani tunabisha hodi DRC. Karibu na mwenyeji wako ni Anold Kayanda.
Mabadiliko ya tabianchi, tishio kwa eneo la bonde la ufa Kenya
Kuongezeka kwa maji kwenye maziwa yaliyo eneo la bonde la ufa nchini Kenya ni jambo ambalo linaendelea kuzua wasiwasi miongoni mwa watu wa maeneo hayo na pia pigo kubwa kwa sekta muhimu ya utalii nchini Kenya. Serikali imekuwa ikiwashauri wale wanaoishi karibu na maeneo hayo kuhama na kujitafutia sehemu salama huku ikitafuta suluhusu ikiwa maji hayo yatazidi kuongezeka siku zinazokuja. Mwandishi wa Kenya Jason Nyakundi amezungumza na mtaalamu wa hali ya hewa nchini Kenya Henry Ndede kutaka kufahamu chanzo ni kipi.
Mkutano wa mabadiliko ya tabianchi umeishaje, na nini kinafuata?
Wakuu wa nchi na serikali zaidi ya 70 , wakiwemo pia viongozi wa kikanda, mameya wa miji mbalimbali na wakuu wa mashirika mbalimbali duniani wamewasilisha hatua wanazotarajia kuchukua ili kupunguza kiwango cha hewa chafuzi ya viwandani na kuzuia dunia kuendelea kuchemka na ongezeko la joto katika mkutano wa matamanio ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi uliomalizika Jumamosi jioni.
Dharura ya mabadiliko ya tabianchi haina chanjo na haiwezi kusubiri tuchukue hatua sasa:UN
Wakuu wa nchi na serikali mbalimbali 77 wameungana na viongozi wa makampuni ya biashara na kutana leo Jumamosi kwa njia ya mtandao kuzungumzia malengo na matamanio ya mabadiliko ya tabianchi na ahadi mpya za kuyatimiza.