09 Februari 2021
Jaridani hii leo Jumanne Februari 09 2021, Flora Nducha anaanzia Msumbiji kumulika msaada wa Umoja wa Mataifa kwa manusura wa kimbunga Eloise, wamejengewa makazi ya muda na huduma za kujisafi na maji safi. Kisha anakwenda Colombia ambako wakimbizi kutoka Venezuela wanazidi kumiminika wakikimbia madhila nchini mwao lakini taifa hilo mwenyeji linarasimisha uwepo wao. Taarifa nyingine ni kutoka Zimbabwe na shirika la FAO.