Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

28 Januari 2021

28 Januari 2021

Pakua

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanza na vipaumbele vya mwaka huu wa 2021 vya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambavyo ni 10. Kisha anakwenda Tanzania kutamatisha sehemu ya pili ya taarifa kuhusu jinsi mashirika ya Umoja wa Mataifa yameleta kujiamini kwa wasichana Angel na Fatma. Kisha anabisha hodi huko Mediteranea ambako twaelezwa kuwa janga la tabianchi ukanda wa Sahel na ghasia pembe ya Afrika vyazidi kusukuma watu kusaka mbinu zote kuvuka baharí na kwenda Ulaya. Makala tunamaliza sehemu ya pili kutoka kwa Mzee Peter Semiga wa Uganda na pia kuna mashinani. Karibu!

Audio Credit
Flora Nducha
Audio Duration
14'3"