Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

08 Februari 2021

08 Februari 2021

Pakua

Hii leo jaridani ni mada kwa kina ambapo Grace Kaneiya kutoka Nairobi Kenya anaangazia wanufaika wa mradi wa shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa, FAO nchini Tanzania katika kuwezesha wakulima mkoani Kigoma kulima maharagwe aina ya Jesca yenye virutubisho. N katika kuelekea siku ya kimataifa ya mikunde tarehe 10 mwezi Februari mwaka huu. Habari kwa ufupi tunaangazia India na maporomoko ya theluji, harakati za kukabili kuenea kwa Ebola iliyotangazwa kuibuka tena Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na mashinani anabisha hodi Lebanon akimulika pia harakati za FAO. Karibu!

Audio Credit
GRACE KANEIYA
Audio Duration
11'11"