Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

23 MACHI 2021

Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Grace Kaneiya anakuletea

-Watu 670,000 wamelazimika kuzikimbia nyumba zao hadi sasa huko Cabo Delgado Msumbiji kufuatia kuendelea kwa mashambulizi dhidi ya raia limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.

- Leo ni siku ya utabiri wa hali ya hewa duniani na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema maji na hali ya hewa ni lila na fila havitengamani

Sauti
13'54"

22 MACHI 2021

Katika jarida la mada kwa kina hii leo kutoka Umoja wa Mataifa Grace Kaneiya anakuletea

-Leo ni siku ya maji duniani na Umoja wa Mataifa umesisitiza kila mtu kutambua thamani ya rasilimali hiyo muhimu ili kuhakikisha watu wote wana fursa ya kuipata kote duniani

-Nchini Sudan Kusini mpango wa Umoja wa Mastaifa UNMISS umeendesha warsha ya siku mbili Yambio na Nzara kwa ushirikiano na serikali ili kuhakikisha vijana, wanawake na jamii wanajikwamua vyema na janga la COVID-19, vita na mabadiliko ya tabianchi

Sauti
12'33"

18 MACHI 2021

Katika Jarida maalum la Umoja wa Mataifa hii leo, Grace Kaneiya anakuletea

-Salamu za rambirambi  zaendelea kutolewa kutoka Umoja wa Mataifa, mashirika yake na viongozi mbalimbali kufuatia kifo cha Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli kilichotokea jana Machi 17

- Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Profesa Kennedy Gastorn amesema Tanzania, Afrika na jumuiya ya kimataifa imepoteza kiongozi mwenye uthubutu na daima ataenziwa John Magufuli

-Wananchi wa Tanzania wamuomboleza Rais wao aliyeaga dunia jana Machi 17

Sauti
12'38"

17 Machi 2021

COVID-19 kuingilia huduma za afya kumechangia vifo 239,000 vya kina mama na watoto Asia Kusini:UN 

UNHCR na wadau wa misaada wazindua ombi la dola bilioni 1.2 kusaidi wakimbizi wa Sudan Kusini

Hali ya wanawake ni hali ya demokrasia – Kamala Harris 

Makala imejikita nchini Tanzania na mashinani ni kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa UNFPA

Sauti
12'45"

16 MACHI 2021

Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo  Grace Kaneiya anakuletea 

-Somalia imefuata nyayo za  nchi zingine za Afrika na kuanza kampoeni ya chanjo dhidi ya COVID-19 baada ya kupokea shehena kupitia mkakati wa COVAX

-Mwaka mmoja baada ya kuzinduliwa kwa mfuko wa kiamataifa wa mshikamano kwa ajili ya COVID-19 WHO inasema umefanya mambo mengi lakini inawasihi wahisani kuendelea kuutunisha 2021

Sauti
12'40"

15 Machi 2021

Jaridani Machi 15 2021 na Grace Kaneiya kwa habari kwa ufupi, makala yetu kwa kina ikiangazia mwanamke kiongozi na ujumbe kutoka kwa Mkurugenzi mtendaji wa UN-HABITAT.

Sauti
11'24"

12 Machi 2021

Hii leo jaridani Ijumaa ya tarehe 12 machi 2021 Flora Nducha anakuletea mada kwa kina ikibisha hodi huko Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kukutana na familia ambayo inamletea mtoto wa kike mwenye umri wa miaka minane baada ya kumuokoa msituni wakati wa mashambulizi kutoka kwa waasi wa kikundi cha ADF. Leo pia ni wasaa wa kujifunza Kiswahili ambapo methali isemayo La kuvunda halina ubani itamulikwa na mchambuzi wetu kutoka BAKIZA.

Sauti
11'55"

11 Machi 2021

Hii leo jaridani ikiwa ni mwaka mmoja tangu shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO litangaze ugonjwa wa Corona au COVID-19 ni janga la afya duniani, tunaanzia nchini Uganda ambako chanjo dhidi ya ugonjwa huo imeanza kutolewa kwa wahuudumu wa afya na wafanyakazi wengine muhimu walio mstari wa mbele. Tutasalia huko huko Uganda kwenye makazi ya wakimbizi  ya Bidibidi ambako walipata ugeni kutoka kwa Kamishna Mkuu wa wakimbizi duniani, Filippo Grandi.

Sauti
13'13"

10 Machi 2021

Leo Jumatano ya Machi 10, 2021 Flora Nducha anaanza na ripoti kutoka Kenya ambako chanjo imeanza kutolewa dhidi ya ugonjwa wa Corona au COVID-19. Kisha anakwenda nchi jirani ya Tanzania ambako Umoja wa Mataifa kupitia kituo chake cha biashara, ITC, umeleta nuru kwa wanawake wajasiriamali wanaokamua chikichi kuwa mafuta ya mawese huko Kigoma. Kutoka Tanzania ni Sudan Kusini ambako walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Bangladesh wanajenga barabara katika mazingira magumu.

Sauti
13'7"

09 Machi 2021

Hii leo jaridani Flora Nducha anamulika harakati za kuondokana na ndoa za umri mdogo duniani akimulika mtoto aliyeolewa na mzee huko nchini Bangladesh, kisha anaangazia mpango wa elimu haiwezi kusubiri ambao umepatiwa dola milioni 1 nchini Niger na mwisho ni taarifa kuhusu madereva wanawake nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati wakifanya kazi na Umoja wa Mataifa. Makala tunakwenda Tanzania ambako Paul Siniga, al maaruf Rio Paul anazungumzia jinsi ushiriki wake wa programu ya HeforShe umemsaidia kuwezesha kujenga usawa wa kijinsia nchini Tanzania na usisahau kuna mashinani, Karibu!