16 MACHI 2021
Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Grace Kaneiya anakuletea
-Somalia imefuata nyayo za nchi zingine za Afrika na kuanza kampoeni ya chanjo dhidi ya COVID-19 baada ya kupokea shehena kupitia mkakati wa COVAX
-Mwaka mmoja baada ya kuzinduliwa kwa mfuko wa kiamataifa wa mshikamano kwa ajili ya COVID-19 WHO inasema umefanya mambo mengi lakini inawasihi wahisani kuendelea kuutunisha 2021
-Miaka 10 ya vita vya Syria shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema nusu ya raia wote wa Syria wamekimbia makwao na madhila bado yanawazogoma
-Makala yetu leo inatupeleka Kenya kuzungumza na mwanamke bondia na mama wa watoto wawili
-Mashinani tuko Mali kwa mlinda amani wa Umoja wa Mataifa mwanamke anayesema alishauriwa asijiunge na jeshi kwa kuwa ni mwanamke.