Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hapa na pale

Mazungumzo ya utekelezaji makubaliano ya amani ya Sudan ya Kusini yanatarajiwa kuanza. Maafisa wa vyeo vya juu wa UM, watakua na duru ya kwanza ya mazungumzo na serekali ya Sudan ya Kusini kutathmini namna ya kutekeleza vizuri zaidi makubaliano ya amani ya Januari 2005 yaliyiomaliza vita vya muda mrefu huko kusini mwa nchi.

Ukuaji wa Idadi ya Watu huko Tanzania

Akizungumza na Redio ya Umoja wa Mataifa, Christopher Mwaijonga mwakilishi mkazi msaidizi huko Tanzania, amesema kwamba, wakati wa mkutano wa Cairo juu ya Idadi ya Watu, 1994, wajumbe walisisitiza juu ya kuwekea mkazo juu ya kuwapatia uwezo wanawake kuamua wakati wanapotaka kupata mimba na kuimarisha afya ya uzazi.