Umoja wa Mataifa kufufua utaratibu wa amani Darfur
Mjumbe maalum wa UM aliyepewa jukumu la kufufua utaratibu wa amani katika jimbo lenye ghasia la Darfur huko Sudan amewasili Sudan wiki hii kuanza mazungumzo mepya .
Mjumbe maalum wa UM aliyepewa jukumu la kufufua utaratibu wa amani katika jimbo lenye ghasia la Darfur huko Sudan amewasili Sudan wiki hii kuanza mazungumzo mepya .
Shirika la wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR na shirika la kimataifa la safari za baharini IMO, yameungana kutoa mwito wa kuchukuliwa hatua zaidi kuzuia vifo vinavyo tokea miongoni mwa watu wanaosafiri kwa maboti katika safari za hatari kabisa kuvuka bahari ya Mediterranean, Ghuba ya aden na kwengineko kujaribu kutafuta maisha bora.
Shirika la watoto la umoja wa mataifa UNICEF limepongeza hatua kadhaa zilizochukuliwa na Misri wiki iliyopita kuondowa mila ya kukeketwa wasichana, baada ya kufariki kwa msichana mwenye umri wa miaka 12 kutokana na kukeketwa.
Afisi ya kulinda amani ya UM huko Ivory Coast imetangaza kwamba itashirikiana na uchunguzi wa kimataifa kutokan na shambulio la roketi wiki iliyopita dhidi ya ndege iliyokua ina msafirisha waziri mkuu Guillaume Soro.
Naibu KM Asha-Rose Migiro Ijumanne alihutubia Kikao cha Saba cha Kimataifa kilichojumuika kwenye mji wa Vienna, Austria kuzingatia taratibu za kurudisha hali ya kuaminiana kati ya wenye madaraka wenye kuendesha serekali na raia wanaotawaliwa.
Majuzi wawakilishi wa mataifa zaidi ya 10 kutoka Afrika Mashariki na eneo la Maziwa Makuu walikusanyika mjini Kampala, Uganda kwenye mkutano wa Shirika la UM dhidi ya Jinai na Madawa ya Kulevya (UNODC), na walizingatia ratiba ya sheria imara dhidi ya biashara ya magendo ya kuteka nyara watu na watoto, na kuwavusha mipaka kutoka makwao na kuwapeleka kwenye maeneo mengineyo kuendeleza ajira haramu, ya lazima, inayotengua kabisa haki za kibinadamu.~~
Wiki hii Baraza la Usalama lilikutana kwenye kikao cha faragha kusikiliza ripoti ya Hedi Annabi, Naibu Mkuu wa Idara ya UM juu ya Operesheni za Amani ambaye alielezea kuhusu ratiba ya siku zijazo inayotakikana kutekelezwa ili kuharakisha upelekaji wa kile kinachojulikana kama ‘furushi zito’ la vikosi vya mseto vya UM na AU katika Jimbo la Darfur, Sudan. Annabi alisisitiza kwenye risala yake juu ya jukumu adhimu la jumuiya ya kimataifa kuikamilisha kadhia hiyo ya amani kidharura.
Shirika la UM la Kulinda Amani Sudan Kusini (UNMIS) limetangaza masikitiko yake kuhusu kifo cha Dktr Majzoub Al Khalifa, Mshauri Mkuu wa Raisi wa Sudan kilichotukia kati ya wiki.
Baraza la Usalama lilipata fursa ya kusikiliza ripoti juu ya matokeo ya ziara ya karibuni ya Tume yake maalumu ambayo ilitembelea Afrika, na ambayo iliongozwa shirika na Balozi Dumisani Kumalo wa Afrika Kusini pamoja na Balozi Emyr Jones-Parry wa Uingereza.
Wajumbe wa Serekali za Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Kenya Usomali na Uganda pamoja na wawakilishi wa UM walikutana kwa mazungumzo ya siku mbili mjini Nairobi (Kenya) wiki hii na walikubaliana kukabili kipamoja vyanzo vyenye kuchochea matatizo ya njaa katika maeneo ya Pembe ya Afrika.