UM unafanya mapitio juu ya utaratibu wa ulinzi wa watumishi wake Afghanistan
Tunaanza na taarifa kuhusu hali ilivyo sasa kwa watumishi wa UM nchini Afghanistan, kufuatia tukio la shambulio la bomu la kujitoa mhanga liliofanyika mapema Ijumatano, kwenye nyumba ya wageni mjini Kabul, ambapo, kwa mujibu wa ripoti za awali, watu wanane waliuawa, ikijumlisha watumishi watano wa UM, na sio sita, kama tulivyotangaza hapo jana.