Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakulima wadogo wadogo wa Tanzania kupatiwa na FAO misaada ya kukuza kilimo na taaluma ya masoko

Wakulima wadogo wadogo wa Tanzania kupatiwa na FAO misaada ya kukuza kilimo na taaluma ya masoko

Shirika la UM kuhusu Chakula na Kilimo (FAO) limeripoti juu ya mradi utakaotumiwa kuimarisha kilimo katika Tanzania, unaokusudiwa kuwasaidia wakulima kuongeza uwezo wa kufikia masoko na kuuza bidhaa zao, hali ambayo itakuza akiba ya chakula nchini.